Rais
wa Sudan Kusini Salva Kiir hatimaye amekubali kikosi cha ziada cha
wanajeshi wa kulinda amani kutokwa Rwanda kitumwe nchini humo.
Rais
Salva Kiir amechukua hatua hiyo jumapili ya tarehe 4 Agosti baada ya
kufanya mazungumzo na ujumbe kutoka kwa Baraza la Usalama la Umoja wa
Mataifa.
Mnamo
mwezi Agosti mwaka 2016 Bwana Kiir alikataa kutumwa kwa wanajeshi hao
takribani 4,000 kutoka mataifa ya kanda, akisema huo ni ukiukaji wa
uhuru wa Sudan Kusini.
Umoja
wa Mataifa -UN umeidhinisha kutumwa kwa wanajeshi hao baada ya kuzuka
upya kwa vita baina ya wanajeshi waaminifu kwa Bw. Kiir na aliyekuwa
Makamu wa rais Dkt. Riek Machar mwezi Julai mjini Juba.
Kikosi
hicho cha ziada kitakuwa na mamlaka zaidi kushinda kikosi cha sasa cha
wanajeshi 13,000 ambacho kimekuwa kikihudumia nchini humo.
Na Hashim Ibrahim (UDSM-SJMC)
0 maoni:
Chapisha Maoni