Alhamisi, 15 Septemba 2016

WATAALAMU WAOMBWA KUTOA ELIMU YA KUKABILIANA NA MAJANGA YA ASILI



index
Na. Sheila Simba,MAELEZO
Jumuiya ya Wanataluma wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDASA) imesema kuwa itaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kukabiliana na majanga ya asili yanayotokea katika maeneo mbalimbali nchini, kutoa msaada wa kitaalam na kuwasaidia waathirika wa majanga hayo.
Aidha, itaendelea kuwahamasisha wadau mbalimbali waendelee kutoa misaada ya kibinadamu ikiwemo vyakula, maji safi na salama, makazi ya muda na madawa kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera ili kuwaepusha na magonjwa ya kuambukiza.
Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya wanajumuiya hao leo jijini Dare Es Salaam na Mtaalamu wa Jiologia wa chuo hicho Dkt.Elisante Mshihu amesema kuwa jumuiya yao itaendelea kutoa elimu na taarifa sahihi kwa umma kupitia tafiti mbalimbali zinazohusu matetemeko ya ardhi kama nyenzo muhimu ya kukabiliana na majanga hayo.
“Matetemeko ni hali ya kawaida duniani na kwa hapa kwetu yamekua yakitokea katika mikoa ya Dodoma,Arusha,Bukoba na Singida ndani ya miaka kumi hivyo ni vyema wananchi wafahamu namna ya kukabiliana nayo yanapotokea”alisema Dkt Mshihu
Dkt.Mshihu amesema elimu na taarifa sahihi ni nyezo madhubuti ya kukabiliana na majanga ya asili kokote Duniani,na kuongeza kuwa uwekezaji katika elimu ni jambo linalohitajika kwa sasa hapa nchini.
“Itabidi elimu ya juu na vyombo vya habari vijengewe uwezo wa kifedha na kitaaluma ili kutimiza majukumyu yake wakati wa kukabiliana na majanga haya ya asili ”alisisitiza Dkt.Mshihu
 Ameongeza kuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki inapaswa kuelekeza nguu zake katika eneo hilo kwani kijiografia na kijiolojia inaonyesha Nchi zote wanachama ziko katika hatari ya kukubwa na majanga ya asili.
Aidha jumuiya hiyo imefungua akaunti katika bank ya NBC yenye jina la UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM SELF INSURANCE,akaunti namba 040103001175 katika tawi la Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam,na kuomba wananchi kujitokeza kwa wingi kuchangia waathirika wa tetemeko lilitokea mkoani kagera hivi karibuni.

0 maoni:

Chapisha Maoni