Alhamisi, 15 Septemba 2016

Denmark, Ujerumani yaonesha nia uzalishaji wa mbolea

nib4
Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Prof. James Mdoe  akielezea fursa za uwekezaji kwenye sekta ya madini nchini



nib1
Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Prof. James Mdoe (aliyekaa mbele) akiongoza kikao kilichoshirikisha mabalozi kutoka katika nchi  za Ujerumani na  Denmark pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC) na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kilichofanyika  hivi karibuni jijini  Dar es Salaam
nib2
Sehemu ya mabalozi na wawakilishi  kutoka katika nchi za Denmark na  Ujerumani  wakifuatilia kwa makini maelekezo yaliyokuwa yanatolewa na Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Prof. James Mdoe ( hayupo pichani)

nib3
Balozi wa Denmark Nchini, Einar Jensen akieleza jambo katika kikao hicho.

nib5
Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo (kushoto) na Kaimu Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Nchini, James Andelile (kulia) wakifuatilia  maelezo yaliyokuwa yanatolewa na Balozi wa Denmark Nchini, Einar Jensen (hayupo pichani)
nib6
Balozi wa Denmark Nchini, Einar Jensen (kushoto) akibadilishana mawazo na Naibu Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo (kulia) kwenye ofisi za Wizara ya Nishati na Madini jijini Dar es Salaam.
nib7
Balozi wa Denmark Nchini, Einar Jensen (kushoto) akisaini kitabu cha wageni kwenye ofisi ya Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo jijini Dar es Salaam
nib8
Kutoka kulia Balozi wa Denmark Nchini, Einar Jensen, Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Nishati, Dkt. Juliana Pallangyo,  Mwakilishi kutoka kampuni  ya Ferrostaal Industrial Projects, Wilfried Wiemann na mwakilishi kutoka  Ubalozi wa Denmark, Mette Melson wakiwa katika picha ya pamoja
……………………………………………………………
Na Greyson Mwase
Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Prof. James Mdoe  amekutana na mabalozi kutoka nchi  za Ujerumani na Denmark  ikiwa ni mwendelezo wa maandalizi kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha mbolea wilayani Kilwa mkoani Lindi.
Kiwanda hicho kinatarajiwa kumilikiwa na kampuni za  Ferrostaal Industrial Projects  ya  Ujerumani, Haldor Topsoe  ya  Denmark na Fauji Fertilizer Limited  ya Pakinstan kwa kushirikiana na  Shirika la Maendeleo ya Petroli Nchini (TPDC)
Akizungumza katika kikao hicho kilichokutanisha pia watendaji kutoka Mamlaka ya  Udhibiti wa Huduma za Nishati naMaji  (EWURA) na TPDC,  Balozi wa Denmark Nchini  Einar Jensen alisema kuwa mara baada ya kukamilika kwa kiwanda cha mbolea, Tanzania itapata manufaa makubwa ikiwa ni pamoja na ajira, fedha za kigeni kutokana na kuuza mbolea nje ya nchi na  hivyo kuinua  uchumi wa nchi.
Wakati huohuo Naibu  Katibu Mkuu wa  Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia Madini, Prof. James Mdoe  alisema kuwa maandalizi kwa ajili  ya ujenzi wa kiwanda hicho bado yanaendelea  ikiwa ni pamoja na ushirikishwaji wa wadau mbalimbali.

0 maoni:

Chapisha Maoni