Kama ulishawahi fikiri kujisaidia kwenye choo kilichotengenezwa kwa dhahabu huu ndo wasaa mzuri wa kutimiza ndoto yako. 
Makumbusho ya sanaa maruufu jijini New York ijulikanayo kwa jina Guggenheim imekizindua choo  maalum kilichopewa jina la ‘America’ katika moja ya vyoo vingi vilivyopo katika makumbusho hiyo. 
Maurizio Cattelan (55) mzaliwa wa nchini Italia ndie mbunifu wa choo hicho kilichotengenezwa kwa dhahabu na ameripotiwa na waandishi wa habari wa nchini Marekani akisema kuwa choo hicho kina dhamira nyingi lakini moja wapo ni  kuonesha kukosekana kwa usawa wa kiuchumi duniani. 
Si mara ya kwanza kwa taswira ya choo kutumika katika sanaa, mnamo mwaka 1917 msanii Marcel Duchamp alitengeneza mfano wa choo cha ukuta maarufu kwa jina la ‘fountain’ ambacho kilileta mabadiliko makubwa kwenye jamii ya sanaa. 
Na Hashim Ibrahim (UDSM-SJMC).
maurizio-cattelanMbunifu wa choo hicho Maurizio Cattelan
golden-throne-toilet