Kampuni ya KFC Kuku Foods Limited Tanzania leo imeanza rasmi kutoa mchango wa vifaa vya braille kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona na kusikia wa shule ya msingi Uhuru Mchanganyiko iliyopo kariakoo. Kampuni ya KFC imedhamiria kutoa msaada kwa shule hii yenye mahitaji maalum kwa kipindi endelevu.
Katika halfa ya makabidhiano ya vifaa maalum kwa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko iliopo Kariakoo, KFC wamesema kuwa vifaa hivyo vitawasaidia wanafunzi wenye mahitaji maalum ambao ni wasio na uwezo wa kuona na wale wasioweza kusikia. Vile vile Msaada huo ni muundelezo wa ushirikiano na uhusiano wa karibu kati ya Kampuni ya KFC na Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko.
Mwaka jana KFC ilitoa mwaliko kwa wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko kuhudhuria ufunguzi maalum wa tawi lao lilipo Kariakoo ambapo Shillingi Milioni Moja zilitolewa kwa ajili ya kusaidia shule hiyo.
dsc_0047Meneja Mkuu wa KFC Tanzania, Louis Venter akizungumza na wanafunzi wa Uhuru Mchanganyiko wa kati wa halfa ya kukabidhi msaada wa vifaa vya braille kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona na kusikia.
Meneja Mkuu wa KFC Tanzania, Louis Venter amesema, “Dhumuni la Mchango wetu ni kusaidia kuboresha mazingira ya kijamii ya watoto hawa. Tunataka mchango huu wa kampuni yetu uwe wa maandalizi ya uzinduzi wa programu maalum iitwayo ‘Add Hope Program’ ya kusaidia jamii nchini Tanzania mwezi Oktoba mwaka huu.”
‘Add Hope Program” ni mradi mahususi uliobuniwa na kampuni mama ya KFC na unaoratibiwa duniani kote ambapo wateja wa KFC wanapata nafasi ya kuchangia maendeleo ya jamii kwa kuongeza pesa kidogo kwenye malipo ya gharama ya chakula walichoagiza.
Mradi wa ‘Add Hope Program’ nchini Afrika ya Kusini ulianzishwa miaka sita (06) iliyopita na umesaidia kupunguza na kutatua matatizo yanayowakumba wananchi wa Afrika ya Kusini kama msaada kwa watoto katika masuala ya lishe kuwasaidia watoto wapate lishe bora, kusoma na kustawi.
Nchini Tanzania mapato yote ya Add Hope ikisha zinduliwa yataenda Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko , ikiwa ni pamoja na michango yote ya baadaye yatakayotolewa na KFC.
dsc_0036Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Bibi Anna Mshana akitoa neno la shukrani kwa KFC Kuku Foods Limited kwa kuwapa msaada wa vifaa vya braille kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona na kusikia.
Kwa upande wa Shule ya Msingi ya Uhuru Mchanganyiko, Mwalimu Mkuu Bibi Anna Mshana ametoa shukrani za dhati kwa kampuni ya KFC kwa msaada wao wa vifaa maalum kwa shule hiyo, “ Elimu ni hazina tosha kwa watoto wetu, vifaa vilivyotelewa na KFC vitasaidia kuhakikisha kuwa wanafunzi wetu wanasoma na kustawi katika mazingira yaliyo sahihi na tunafurahi kuwa na rafiki wa karibu KFC,” alisema.
dsc_0034Mkuu wa Kitengo cha Wanafunzi Walemavu katika Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Ahmed Abdallah akielezea jinsi msaada huo unavyoweza kuwasaidia kupunguza mapungufu ya vifaa yaliyokuwa yanawakabili.
dsc_0073Mwanafunzi wa Uhuru Mchanganyiko, Haji Zuberi akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wanafunzi wenzake baada ya kupewa msaada na vifaa vya braille kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona na kusikia.
dsc_0056Meneja Mwendeshaji wa KFC Kuku Foods Limited, Paul Wenger akimkabidhi msaada wa vifaa vya braille, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko, Bibi Anna Mshana.
dsc_0058
dsc_0064
dsc_0053Wafanyakazi wa KFC Kuku Foods Limited wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi Uhuru Mchanganyiko baada ya kukabidhi msaada wa vifaa vya braille kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona na kusikia.
dsc_0022Baadhi ya wanafunzi wa Uhuru Mchanganyiko waliohudhuria halfa ya kupokea msada wa vifaa vya braille kwa wanafunzi wenye ulemavu wa kuona na kusikia kutoka KFC Kuku Foods Limited.
dsc_0021