Jumanne, 13 Septemba 2016

WABUNGE WAFURAHISHWA NA KASI YA NIDA KATIKA UTOAJI VITAMBULISHO VYA TAIFA


Posted by Esta Malibiche on Sept14.2016 in News
kaf3
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Iramba Magharibi Mhe. Mwigulu Nchemba akipata maelezo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati NIDA; Bi. Rose Mdami mara baada ya kupokea kitambulisho chake cha Taifa.
kaf1

Mbunge wa Igunga Dkt. Dalaly Peter Kafumu akiwa amejawa na furaha baada ya kupokea Kitambulisho chake kipya chenye saini Kinachotolewa na NIDA katika zoezi la ugawaji wa vitambulisho hivyo kwa waheshimiwa Wabunge, Bungeni Dodoma.
kaf2
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi na Mbunge wa Iramba Magharibi Mheshimiwa Mwigulu Nchemba; akiweka saini katika orodha ya majina ya wabunge baada ya kupokea Kitambulisho chake kipya chenye saini Bungeni Dodoma. Kushoto ni Afisa wa Mifumo ya Kompyuta NIDA Bi. Zainabu Mavere.


kaf4
Mhe. Azzan Mussa Zungu Mbunge wa Jimbo la Ilala (wapili kulia) mara baada ya kuchukua kitambulisho chake chenye saini Bungeni Dodoma. Kulia ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Hifadhi Hati Bi. Rose Mdami, kushoto ni Afisa Usajili NIDA Bw. Thadei Minja na wa pili kushoto ni Afisi Usajili wa Wilaya ya Dodoma Mjini Bwana Khalid Mrisho.
kaf5
Mbunge wa Singida Magharibi Mh. Elibariki Emmanuel Kingu akiwa mwenye furaha baada ya kuchukua Kitambulisho chake chenye saini leo bungeni Dodoma, ambapo NIDA imeanza kugawa vitambulisho vyenye saini kwa waheshimiwa Wabunge. Kushoto ni Afisa Usijili Wilaya ya Dodoma Mjini Bw. Khalid Mrisho.
kaf6
Mh. Seif Khamis Said Gulamali Mbunge wa Jimbo la Manonga kwa furaha akionyesha kitambulisho chake kipya chenye saini baada ya kupokea kutoka kwa Afisa Usajili wa NIDA wilayani Dodoma Mjini Bwana Khalid Mrisho Bungeni Dodoma.
kaf7
Afisa wa Jeshi la Polisi, akithibitisha kupokea kitambulisho chake kwa kuweka saini kwenye daftari maalumu la kumbukumbu, baada ya kuchukua Kitambulisho chake leo bungeni Dodoma. Zoezi la ugawaji wa Vitambulisho vyenye saini limeanza katika ofisi za
……………………………………………………
Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo wamekuwa miongoni mwa wananchi walioanza kuchukua Vitambulisho vipya vya Taifa vyenye saini; kufuatia utaratibu uliotangazwa hivi karibuni na Nida wa kuanza kugawa vitambulisho vipya kwa makundi mbalimbali waliokamilisha taratibu za usajili 
            Shughuli ya kugawa Vitambulisho vya Taifa kwa Waheshimiwa Wabunge imeanza rasmi leo bungeni; pamoja na kuendelea kuwasajili wabunge ambao kwa sababu moja au nyingine hawakusajiliwa wakati wa zoezi la awali la usajili
            Mbali na waheshimiwa Wabunge; wengine ni wafanyakazi wa Bunge na watumishi katika taasisi na Wizara mbalimbali ambao walisajiliwa katika utaratibu wa kawaida wa Usajili. Zaidi ya waheshimiwa Wabunge 240 wanakusudiwa kupatiwa vitambulisho vyao.

0 maoni:

Chapisha Maoni