Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla ameagiza waajili wote nchini kutoajili wataalamu wasio sajiliwa na wataalamu wa Baraza la Maabara za Afya nchini ili kuepuka kuajili wataalam hewa.
Dk. Kigwangalla ameyasema hayo leo wakati wa uzinduzi wa Baraza la Wataalamu wa Huduma za Maabara za Afya tukio lililofanyika Jijini Dar es Salaam ambapo Naibu Waziri alikuwa mgeni rasmi huku akitoa vyeti kwa wajumbe wa Baraza hilo waliomaliza muda wao pamoja na wajumbe wapya.
Akipongeza Baraza hulo la Maabara, amesema kuwa licha ya kuwa ni la siku nyingi, ambapo amelitaka kuhakikisha wanashirikiana na Mamlaka zingine husika kusimamia ubora wa wataalamu kusimamia vyuo husika katika kuwapata wataalam hao.
Pia amewataka wataalamu wa Maabara waliosajiliwa kwa sheria ya 12 ya 1997, wajisajili tena upya kwa sheria mpya ya namba 22 ya mwaka 2007 kama ilivyoelekezwa ili wapate vyeti vipya.
Mwisho amewaagiza wataalamu woye wa maabara waliosajiliwa wanalipia ada ya usajili kila mwaka ili kuendelea kupata kibali cha kuendelea kutoa huduma cha maabara kwa mwaka mzima ili baraza hilo liweze kujiendesha.
“Ili muwe wataalam, lazima muwe na chombo kama hichi. Hivyo katika msingi huo nyie wataalum wenyewe mutakiwa kujiongeza katika kuhakikisha munapata fedha kwa kuchangia/kuchangishana muweze kujindesha kama yalivyo mabaraza mengine” amesema Dk.Kigwangalla.
Baraza la Wataalamu wa Maabara za Afya, ni chombo cha kisheria kilichowekwa na Serikali ili kuwatambua na kuwasajili Wataalamu wa Maabara za Afya ya Binadamu, kusimamia ubora wa utoaji wa huduma za uchunguzi wa magonjwa ya binadamu, kuchukua hatua za kisheria kwa wakiukaji wa sheria, na kushauri Serikali katika kuboresha huduma za maabara kwa wagonjwa.
Taaluma ya Maabara za Afya ni kati ya taaluma nyeti katika tasnia ya tiba na Sekta ya Afya kwa ujumla.  Kwa kuwa ndio inayotoa dira ya tiba sahihi kwa wagonjwa wanaohitaji tiba.  Isitoshe, magonjwa ya milipuko na magonjwa yanayoibukia, mfano homa ya bonde la ufa, Dengue na Ebola yanahitaji taaluma ya maabara kuweza kuyabaini na kuyadhibiti. 
Aidha, tafiti nyingi za magonjwa ya binadamu duniani zinahitaji taaluma ya Maabara kuweza kupata ushahidi wa kisayansi ili kupata tiba sahihi kwa wagonjwa na kudhibiti au kupata kinga kwenye jamii.  Hivyo, Baraza hili lina jukumu kubwa la kuhakikisha kuwa, taaluma hii inakuwa na ubora unaostahili kwa faida ya Taifa zima kwa ujumla.
Katika kutekeleza agizo hilo, Wizara itandelea kuongeza nguvu katika juhudi za kufuatilia vyuo vyote vilivyohusika na vyeti vya kugushi.  Ambapo ameomba Kamisheni ya Vyuo Vikuu (TCU) na Taasisi ya Taifa ya Elimu ya Ufundi (NACTE) kuwa makini katika usaili na ufuatiliaji wa ubora wa taaluma zinazotolewa katika vyuo wanavyovisimamia na kuvisajili. 
“Tushirikiane kuhakikisha kuwa hakuna Taasisi au Mtu Binafsi, atakayefungua au atakayetoa mafunzo ya taaluma bila kusajiliwa  kisheria.  Aidha, nawakumbusha waajiri wote wa Sekta ya Umma na Sekta Binafsi, wazingatie kutowaajiri watalaamu ambao hawajasajiliwa” alimalizia Dk. Kigwangalla.


Kigwa
 Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Mohamed Bakari Kambi akifungua mkutano huo wa uzinduzi wa Baraza la Wataalamu wa Huduma za Maabara za Afya nchini. Kushoto kwake ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla
dsc_2263
Baadhi ya wajumbe wa Baraza la wataalam wa Maabara za Afya nchini waliomaliza muda wao wakifuatilia tukio hilo
dsc_2265Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia tukio hilo
dsc_2275Baadhi ya wajumbe wapya wa Baraza hilo wakijitambulisha
dsc_2268 dsc_2271 dsc_2269 dsc_2326Meza kuu: Dkt. Magreth Mhando, Mkurugenzi wa Idara ya Tiba, Naibu Waziri wa Afya Dk.Kigwangalla na Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Mohamed Bakari Kambi katika tukio hilo
dsc_2335Picha ya pamoja ya Wajumbe wa Baraza la Wataalam wa Maabara za Afya wakiwa na mgeni rasmi Naibu Waaziri wa Afya Dk.Kigwangalla.
dsc_2359 dsc_2366 Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na waandishi wa Habari juu ya hali ya wataalamu wa Maabara nchini. (Picha zote na Andrew Chale