Jumapili, 25 Septemba 2016

WALIMU WALIPWA STAHIKI ZAO ARUSHA


Posted by Esta Malibiche on Sept25.2016 in NEWS
indexNa Mahmoud Ahmad,Arusha
Jumla ya Tsh.154 milion wameapatiwa waalimu 701wa shule za msingi na sekondari kutoka kwenye fedha ambazo zilitakiwa kulipa posho za nauli na simu za madiwani wa jiji la Arusha.
Akiongea na wanahabari ofisini kwake jijini hapa mkuu wa wilaya ya Arusha mjini Gabriel Daqqaro alisema kuwa kutokana na malimbikizo ya fedha za likizo,kufiwa,nauli, uhamisho waliokuwa wanadai walimu ndio maana tumeamua kuwalipa ili waweze kufanyakazi ya kufundisha watoto wetu kwa moyo.
Daqqaro alisema kuwa baada ya kikao na mkuu wa mkoa Mrisho Gambo na waalimu wa shule 48 za jiji la Arusha, na kuagizwa kuhakikisha walimu wanalipwa stahiki zao ndani ya wiki mbili na agizo hilo tumelitiza na walimu wamelipwa fedha zao.
Alisema kuwa fedha zilizolipwa waalimu hao tumezitoa kwenye fedha zilizokuwa wakijilipa madiwani posho za usafiri na posho za simu na kuzielekeza fedha hizo kutatua kero ya waalimu na mwisho wa siku vijana wetu wapate elimu stahiki bila manung’unuko kutoka kwa waalimu.
”Hapa napenda tusiingize ushabiki wa kisiasa katika hili na tuache kuzusha maneno maneno yanayaashiria uvunjifu wa amani kama kweli fedha hizo wanadai walifuta iwaje leo waendeleze maneno”alisema DC Daqqaro.
Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano ipo kuhakikisha wananchi walio wengi wanaondolewa kero zao kwa wakati na kuondosha kabisa kero mbali mbali ndani ya jamii ikiwemo waalimu kupewa stahiki zao kwa wakati.
Akawataka waalimu hao kuhakikisha malengo ya mkoa kuongeza ufaulu yamefikiwa kwa kufanyakazi kwa moyo huku serikali ikiendelea kumalizia malalamiko mbali mbali ya waalimu wa mkoa wetu.
Malipo hayo ya waalimu 701yametokana na agizo la mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akiwataka dc na mkurugenzi wa jiji la Arusha Athman kihamia kuhakikisha malalamiko ya waalimu walioyatoa kwenye mkutano wao yanatekelezwa ndani ya wiki mbili .

0 maoni:

Chapisha Maoni