Alhamisi, 29 Septemba 2016

SERIKALI IMETOA BIL.2 KUJENGWA GATI NYAMISATI

Posted by Esta Malibiche on Sept29.2016 in NEWS
kibi2
Na Mwamvua Mwinyi,Pwani
SERIKALI imeanza kutenga fedha sh. bil.2 ambazo tayari zimeshapelekwa wizara ya ujenzi ,ili kujengwa gati itakayohudumia wananchi wa Nyamisati wilayani Kibiti,Mafia na Rufiji.
Aidha serikali inafanya utaratibu wa kutafuta boti moja kubwa ambayo itaweza kuhimili nguvu ya maji na kukatisha katika maeno hayo.
Waziri mkuu Kassim Majaliwa aliyazungumza hayo kwenye mkutano wa hadhara wa wananchi huko Nyamisati wilaya ya Kibiti,mkoani Pwani.
Alisema serikali imedhamiria kuimarisha na kuondoa kero iliyopo kwasasa wanayopata wananchi baada ya gati la awali kubomoka kutokana na kushindwa kuhimili nguvu ya maji.
Alisema kipindi cha nyuma halmashauri yenyewe ilijenga gati hiyo kwa kiasi cha sh.mil.400 lakini ilibomoka kutokana na wingi wa maji .
“Wilaya ya mafia waliizungumzia vizuri sana kuwa ni tumaini lao,na mimi nilidhani watazungumzia kitu kipya lakini wameipenda sana Nyamisati,kwahiyo wakizungumza kitu ambacho nakifahamu,lakini serikali inajua gati hii inatumika na wilaya yote ya Mafia hivyo ni lazima tuimarishe”alisema Majaliwa.
Majaliwa alisema kwasasa watu wanapata shida ya kukwida nguo ndipo upande boti lakini anatarajia baada ya kujengwa gati hiyo kero hiyo itabaki historia.
Alieleza kuwa gati hiyo itajengwa na fedha imeshatengwa na kupelekwa wizara ya ujenzi waende kushughulikia kuijengajenga kwani barabara ni kubwa na gati ni tegemeo la wilaya yote ya Mafia.
Hata hivyo alisema mbinge wa jimbo la Kibiti,Ally Ung’ando ,amekuwa akisema mara kwa mara na kung’ang’ania juu ya suala hilo hivyo majibu yake ni hayo wananachi wawe na subira.
Alisema masuala ya gati yanaenda sambamba na miundombinu ya barabara ambapo alikiri kwasasa serikali ilishindwa kutenga fedha kwa ajili ya barabara ya Bungu-Nyamisati.
Alisema kwasasa wataiimarisha kwa kiwango cha changalawe ili iweze kutumika wakati wote licha ya hamu ya wilaya kutaka ijengwe kwa kiwango cha lami barabara hiyo.
Majaliwa alieleza kwa mwaka huu,wameendelea kulipa madeni ya barabara kuu ikiwemo Dar es salaam,Lindi,Masasi kwani mkandarasi alikuwa akidai fedha kutoka Masasi ,Tunduru,Namtumbo,Songea, Mbinga na Mbababei.
“Kuna barabara inayotoka Mbeya kwenda mikoa ya Songwe ,Tunduma,Sumbawanga ,Katavi hadi Uvinza- Kigoma kuunganisha barabara ya kutoka Kigoma –Tabora ambayo tayari ina lami ,tunafanya hivyo ili kuwezesha barabara mzunguko nchi nzima na zoezi hilo tutalikamilisha “
“Tunafanya hivyo kwasababu ya kuijenga barabara ya kutoka Dodoma kupitia Kondoa kwenda Babati mjini kwahiyo watu wa Dodoma watakwenda Arusha kwa ukaribu na wa Arusha watakwenda makao makuu ya nchi kwa ukaribu zaidi”
‘Pia kuimarisha barabara kutoka Kigoma kwenda Kasulu,Kibondo na kutokeza Nyakanazi ili kuunganisha barabara ya kutoka Ngara,Bukombe,Kahama,Shinyanga hivyo huo ndio mkakati wa serikali.
Majaliwa alielezea kuwa mpango ni kukamilisha barabara zote kuu nchini kwa kiwango cha lami ,kisha za ndani ya mikoa ambazo hazijakamilika  na baada ya hapo za wilaya ikiwemo Bungu-Nyamisati,Nyamwage-Utete na Kilimani –Mloka.
Aliwahidi wananchi na mbunge wa Kibiti kuwa barabara hizo ni muhimu hivyo serikali haiwezi kuwaangusha .
Majaliwa alisema wanaendelea kuwabana wabadhilifu wa fedha na wafanyabiashara kulipa kodi ili fedha hizo ziweze kuwatumikia wananchi kwenye huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo kuboresha na kuimarisha miundombinu ya barabara.
Awali mbunge wa viti maalum na mwenyekiti wa jumuiya ya wanawake mkoani Pwani,Zainab Vullu alieleza kero kubwa ya ukosefu wa gati hali inayosababisha wananchi kupata kero.

0 maoni:

Chapisha Maoni