Alhamisi, 15 Septemba 2016

MATUKIO KATIKA PICHA KUTOKA BUNGENI DODOMA LEO

Posted by Esta Malibiche on Sept15.2016 in SIASA

ug1

Spika wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiingia katika ukumbi wa Bunge kuongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
ug2
Spika wa Bunge la Jmahuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai akiongoza kikao cha saba cha bunge la kumi na moja ambapo pia alisema kiasi cha shilingi milioni themanini na tano na laki tano zimechangwa kutokana na makato ya posho ya siku moja yawabunge kwa ajili ya kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera
ug3
Waziri wa Habari, utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (MB) akimueleza jambo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, kazi, Ajira, Vijana na watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (MB) picha juu ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais-Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiteta jambo na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angela Kairuki wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
ug4
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani Jafo (MB) akijibu swali bungeni ambapo alisema kuwa serikali itaendelea kupeleka fedha katika serikali za mitaa kwa kuzingatia hali ya makusanyo ya kila mwezi.
ug5
wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Hussein Mwinyi akijibu swali bungeni ambapo alitoa wito kwa wabunge kuisaidia kutoa elimu kwa wananchi waliovamia maeneo ya jeshi kuondoka ili kusaidia kupunguza migogoro ya ardhi baina ya jeshi na wananchi, wakati wa kikao cha saba cha bunge la kumi na moja leo mjini Dodoma.
ug6 ug7
Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akijibu swali bungeni ambapo alisisitiza kuwa Serikali inatekeleza program
ug8
Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mhe. Joseph Haule akiuliza swali bungeni kutaka kujua mikakati ya serikali katika kutatua migogoro baina ya wakulima na wafugaji inayopelekea mauaji ya raia ambapo Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi alisema Serikali itawachukulia hatua kali za kisheria wale wote wanaohusika na mauaji ya raia nchini hasa ikiwemo wanaohusika kwenye migogoro hii.
PICHA NA HASSAN SILAYO-MAELEZO

0 maoni:

Chapisha Maoni