Linapokuja
suala la wanamitindo kutunisha akaunti zao za benki kutokana na
kushiriki vyema katika mitindo basi Gisele Bundchen amekua ndio kinara
kwa takribani miaka 14 ambapo jarida la Forbes linamtaja kuwa katika
orodha ya wanamitindo wanaopokea pesa za madafu nyingi kuliko wote akiwa
anashikilia namba moja.
Gisele
anazidi kufanya maajabu ambapo hata mwaka huu wa 2016 amekuwa wa kwanza
ambapo jumla ya mapato aliyoyapata ni takribani dola milioni 30.5.
Gisele Bundchen.
Wadau
wa mitindo wamesema kuwa utawala wa Gisele kwenye chati hizo unakaribia
kufika mwisho wake siku si nyingi baada ya takwimu mpya za jarida la
Forbes kuwataja Kendall Jenner na Gigi Hadid kuwa ndio vinara wadogo
wanaokuja juu kwa kasi katika chati za tasnia ya mitindo.
Jenner
amepanda kutoka nafasi ya 16 hadi nafasi ya 3 mwaka huu akiyazidisha
mapato yake kutoka dola milioni 4 hadi dola milioni 10 kutokana na
mikataba mbalimbali.
Kwa
upande mwingine Gigi Hadid anatajwa kuingia katika orodha hiyo kwa mara
ya kwanza na kushika nafasi ya 5 kutokana na mikataba ya Maybelline na
Tommy Hilfiger iliyomuingizia mapato ya takribani dola milioni 9.
Na Hashim Ibrahim (UDSM-SJMC)
Gidi Hadid.
Kendall Jenner.
0 maoni:
Chapisha Maoni