Kwa
siku za karibuni katika michezo ya kimataifa kumekuwepo na taarifa
ambazo zinamhusu mshambuliaji wa Atletico Madrid na timu ya taifa ya
Ufaransa, Antoine Griezmann kuwa anaweza kujiunga na Manchester United
baada ya msimu wa 2016/2017 kumalizika.
Taarifa
kutoka mtandao wa The Manchester United News, zimeeleza kuwa staa huyo
amewambia Man United kuwa kama wanamhitaji basi wafanye mazungumzo na
kocha wa klabu yake, Diego Simeone kwani ndiye ambaye anajua hatma yake
ya soka klabuni hapo.
“Jambo
lolote ambalo linaihusu Atletico basi anaachiawa Simeone, nilimuita
kabla ya kuongeza mkataba wangu, na alinihakikishia kuwa nitaendelea
kusalia klabuni. Ninajifuza mambo mengi kutoka kwake, na nina furaha
kuwa Hispania,” alisema Griezmann.
Mchezaji
huyo mwenye miaka 25 alijiunga Atletico Madrid mwaka 2014 akitokea Real
Sociedad na mwezi Juni aliongeza mkataba mwingine na klabu yake ambao
utamwezesha kusalia klabuni hapo hadi mwaka 2021.
0 maoni:
Chapisha Maoni