Mwanamuziki
maarufu duniani anayetamba na kibao chake cha Lemonade, aamua kufanya
sherehe yake ya kuzaliwa ndani ya Ikulu ya Marekani, akiwa na mtoto wake
Blue Ivy.
Beyonce
anayetimiza miaka 35, aliamua kujumuika na mke wa Rais wa Marekani
Michelle Obama na watoto wake Malia na Sasha, nyumbani kwao Ikulu
Washintong DC Marekani, lakin Rais wa Marekani Barack Obama hakuweza
kujumuika pamoja nao kutokana na kuwa katika ziara zake za kikazi nchini
China.
Mwanadada
aliyetamba kwa kuondoka na tuzo nane katika tuzo za VMA hivi karibuni,
alionekana katika maeneo ya Marryland akiwa na mtoto wake wakielekea
katika sehemu walipoandaliwa kwaajili ya hafla hiyo na Michelle Obama
“Camp David”.
“Niukweli
dhahiri kwamba Beyonce ana weza kabisa kualikwa kushehereka sherehe
yake hiyo na familia ya Obama kwani wakati wa sherehe ya kuzaliwa ya
Rais Barack Obama, Beyonce na mumewe Jay Z walikua kati ya wageni
walioalikwa na aliweza kutumbuiza katika sherehe hiyo.” Alisema mmoja wa
wasemaji wa Ikulu ya Marekani.
Aidha
mitandao ya kijamii imekua ikifurika kwa salamu za pongezi kwa
mwanadada Beyonce toka kwa mashabiki wake wakiwa na haya ya kusema : –
0 maoni:
Chapisha Maoni