Posted by Esta Malibiche on Sept10.2016 in News
Na Mahmoud Ahmad Monduli
Baraza la madiwani .limewafukuza kazi watumishi wawili na wawili kupewa.onyo kali huku
likiridhia mwanasheria wa halmashauri hiyo kurejea kazini baada ya
kushinda kesi
Akiwataja watumishi hao Mwenyakiti wa baraza.la madiwani
isack Joseph Kopriano ameeleza kuwa wamejadiliana kwa muda mrefu
kuhusiana na watumishi hao na ndipo wakafikia maamuzi ya kuwafukuza kazi
Kitundu Mkumbo na mwenzake Leonard Lukwavi .na kuwapa.onyo kali
wenzao wawili kutoka kwenye idara ya Ardhi.ambapo.waliridhia mwanasheria
wa halmashauri hiyo Leonard Haule kurudi kazini baada yakushinda kesi
iliyokuwa ikimkabili.
Hatua hiyo imetokana
watumishi waliofukuzwa kukutwa na makosa mawili kila.mmoja.hali
iliyopelekea baraza kuchukua uamuzi wa kuwafuta kazi,ambapo wenzao
wawili makosa yao wao walipewa onyo kali.
Kwa upande wa
mwanasheria alifikishwa.mahakamani na takukuru lakini aliweza.kushinda
kesi hiyo na kukosa kuwa na tuhuma ambazo zilizokuwa zinamkabili hivyo
baraza likaridhia kumrudisha kazini.
Kwa upande
wake.mkurugenzi wa halmashauri hiyo Stephen Ulaya alisema.kuwa
atayafanyia.kazi.maagizo aliyopewa na mkuu wa wilaya bila kumuonea.mtu
aibu wala.kumpendelea wala kumuonea mtu na ataongoza halmashauri kwa
kufiata kanuni na taratibu.
Aidha mkurugenzi huyo
aliwataka watumishi hususani watendaji wa Vitongoji,vijiji na kata
kuhakikisha wanafuata taratibu na kanuni kwa.kuitisha mikutano ya
wananchi kwa.wakati na yeyote atakayebainika kwenda kinyume na hilo
sheria itachukua mkondo wake..
Hata hivyo.aliwataka
madiwani kuwapa.ushirikiano watumishi.hao.vitongoji vijiji na kata ambao
wamekuwa.wakifanya kazi kwa.mazowea ili kuhakikisha wananchi.wanapata
hudumakwa.wakati na kutoa michango yao kwaajili ya maendeleo ya wilaya
hiyo.
“Monduli ni yetu sote
lazima tufanye kazi kwa.bidii kuhakikisha wananchi wanapata huduma
kwa.wakati, na sintamuonea mtu wala.aibu,mtumishi yeyote atakayekiuka
sheria za utumishi na utawala ,ili kuhakikisha maendeleo.yanawafikia
wananchi.kwa wakati, alisisitiza ulaya“
Alibainisha kuwa yeyote
atakayekutwa miradi ya maendeleo ipo chini ya kiwango na katika mradi
husika ambapo ambaye hatafanya mkutano mkuu wa wananchi katika
kitongoji,kijiji na kata kwa.wakati atakuwa amejiondoa.mwenyewe kwani
utumishi ni pamoja na kujali kanuni na taratibu za kazi yako.
0 maoni:
Chapisha Maoni