Posted by Esta Malibiche on Sept 7.2016 in SIASA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wananchi waliojitokeza kumsalimia aliposimama Nangurukuru, wilaya ya Kilwa mkoani Lindi wakati akiwa njiani kuelekea
mkoa wa Mtwara ambapo atakuwa na ziara ya kikazi ya siku nne.
Sehemu ya Wakazi wa Nangurukuru mkoani Lindi wakishangilia ujio wa Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.mkoa wa Mtwara ambapo atakuwa na ziara ya kikazi ya siku nne.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wananchi waliojitokeza kumsalimia alipowasili kwenye ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambapo atakuwa na ziara ya kikazi ya siku nne.
Makamu wa Rais Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akiwasalimia wananchi katika mji wa Nangurukuru Wilaya ya Kilwa waliojitokeza kwa wingi wakati akipita kuelekea Mkoani Mtwara kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu.
Makamu wa Rais Mh. Mama Samia Suluhu Hassan akiwapungia mkono wananchi alipokuwa akiwasalimia wananchi katika mji wa Nangurukuru Wilaya ya Kilwa waliojitokeza kwa wingi wakati akipita kuelekea Mkoani Mtwara
Baadhi ya wananchi aliojitokeza kumlaki Makamu wa Rais Mama Samia Hassan Suluhu wakati akipita kwenye mji wa Nangurukuru wilayani Kilwa mkoa wa Pwani.
………………………………………………….
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema
serikali itatuma kikosi maalum cha kukabiliana na uvuvi haramu
unaoendelea katika bahariili kudhibiti na tatizo hilo ambalo limeathiri
sana mazalia ya samaki na
kuchangia kupungua kwa samaki baharini.
kuchangia kupungua kwa samaki baharini.
Makamu
wa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kauli hiyo 7-Sept-2016 wakati
akisalimiana na wananchi wa Nangurukuru wilayani Kilwa mkoani Lindi
ambao walijitokeza kumsalimia wakati akielekea mkoani Mtwara katika
ziara yake ya
kikazi ya siku NNE mkoani huo.
kikazi ya siku NNE mkoani huo.
Makamu
wa Rais amesema katika kuhakikisha kazi hiyo inafanyika vizuri serikali
pia itatuma wataalamu wa mazingira ambao watafanya tathmini ya
uharibifu wa mazingira katika bahari ili kujua uharibifu uliofanyika na
kuchukua hatua ya kukabiliana na hali hiyo.
Ameeleza
kuwa serikali itachukua hatua hizo ili kuinusuru bahari kwa sababu
imekuwa ni chanzo kizuri ya mapato kwa wananchi kutokana na shughuli za
uvuvi na shughuli nyingine zikiwemo za utalii.
“Bahari
yetu ndio mapato yetu, bahari yetu ndio maisha yetu tumeitumia vibaya
mapato yamepungua na maisha hayawi mazuri hivyo ni muhimu tuitunze ili
iendelee kutulea kwa manufaa mazuri.”
Kuhusu
uboreshaji wa huduma za afya kwa wananchi wa Kilwa, Makamu wa Rais
Samia Suluhu Hassan amesema serikali inaendelea kuchukua hatua madhubuti
zinazolenga kuhakikisha wananchi wote nchini wanapata huduma bora za
afya katika ngazi zote.
Amesema
mpango huo wa uboreshaji wa huduma za afya kwa wananchi nchini utaenda
pamoja na utoaji wa elimu bora wa wanafunzi kote nchini chini ya mkakati
wa serikali wa kutoa elimu bure kuanzia wanafunzi darasa la kwanza
hadi kidato cha nne.
Katika
ziara yake mkoani Mtwara, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Samia Suluhu Hassan kesho 8-Sep-16 atazindua jengo la ofisi za
Tume ya Maadili ya Uongozi wa Umma Kanda ya Kusini na kukagua miradi
mbalimbali ya maendeleo
mkoani humo.
Makamu wa Rais tayari
amewasili mkoani Mtwara na kupokelewa na Viongozi mbalimbali wa mkoa huo
wakiongozwa na Mkuu wa mkoa wa Mtwara Halima Dendego pamoja na Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora
Angela Kairuki.mkoani humo.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
0 maoni:
Chapisha Maoni