…………………………………..
TUME
ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Pemba imewashauri wananchi kuwatumia
viongozi wa Dini pamoja na mabaraza ya wazee katika kutafuta suluhisho
na matendo ya hujuma yanayoendelea kutokea Kisiwani humo .
Ushauri
huo umetolewa na Msaidizi Kamishna wa Tume hiyo Pemba , Suleiman Salum
wakati akizungumza na mwandishi wa habari hizi huko ofisini Kwake na
kusema ofisi yake imesikitishwa na matendo hayo .
Amesema
kwamba suluhisho na matendo hayo inaweza kupatikana iwapo jamii
itawatumia viongozi wa dini pamoja na mabaraza ya wazee katika kutafuta
ushauri na suluhisho la matendo ya kuhujumiwa mali za wananchi .
Aidha
amefahamisha kuwa matendo hayo yanakwenye kinyume na msingi ya haki za
binadamu na utawala bora kwani yanaweza kusababisha kutowekwa kwa amani
ya nchi .
“Ni
vyema jamii kuwatumia viongozi wa dini pamoja na mabaraza ya wazee
kutafuta suluhisho la matendo ya hujuma yanaendelea kutokea kwa baadhi
ya maeneo ya Kisiwani cha Pemba ”alifahamisha.
Akizungumza
utendaji kazi wa Tume hiyo Kisiwani hapa , alisema kwamba bado wananchi
hawajakuwa na mwamko wa kitumia kwani tangu ilipopfunguliwa Septemba
mwaka 2015 , wamepokea lalamiko moja la ukiukwaji wa haki za binadamu .
Pia
amefahamisha kuwa licha ya Tume kutoa elimu kupitia Ofisi za wakuu wa
Wilaya na Mikoa , lakini bado mwitikio wa wananchi ni mdogo na kutumia
fursa hiyo kuwataka wananchi kuwasilisha malalamiko yao ili yafanyiwe
kazi .
“Tunatoa
elimu kupitia vyombo vya habari , masheha pamoja na Ofisi za wakuu wa
Wilaya na Mikoa , lakini mwitikio bado ni mdogo , hivyo nawaomba sana
wananchi waitumia ofisi yetu kuwasilisha malalamiko yao ”alishauri .
Baadhi
ya wananchi waliozungumza na mwandishi wa habari hizi , wamesema
wanahitaji elimu juu ya kuitumia Tume hiyo , kuomba watendaji wake
kufika maeneo ya vijini kwa ajili ya kutoa elimu .
Hata
hivyo Msaidizi wa Tume hiyo inakabiliwa na changamoto ya upungufu wa
wafanyakazi jambo ambalo linawakamishwa kuweza kuyafikia maeneo yote ya
Kisiwani cha Pemba .
0 maoni:
Chapisha Maoni