Jumatano, 1 Juni 2016



mbunge  wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu (kulia) akimpokea  waziri wa Kilimo ,Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba alipofanya ziara ya  kikazi wilaya ya Manyoni jana
Waziri Nchemba  akisalimiana na mbunge Nyalandu (kulia)
Waziri  wa  kilimo ,mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  akiwa ameongozana na viongozi mbali mbali  kuingia  ukumbi wa mkutano kati yake na wakulima wa Tumbaku Manyoni
Mbunge Lazaro  Nyalandu kulia akiwa na waziri wa Kilimo ,mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba wakati akisaini kitabu cha  wageni  ofisi ya mkuu wa wilaya ya Manyoni mkoani Singida
Waziri Nchemba  akiingia ukumbi wa mkutano kati yake na  wakulima wa Tumbaku manyoni
Wakulima wa Tumbaku  wakisalimiana na waziri Nchemba 
Baadhi ya madiwani  wakulima wa Tumbaku manyoni wakimpokea  waziri Mwigulu Nchemba
Baadhi ya  wakulima wa Tumbaku  wakiwa  ukumbi wa mkutano kati yao na waziri Nchemba
Mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu  akitambulisha  viongozi mbali mbali kabla ya  mkutano wa  wakulima wa Tumbaku kuanza
Waziri wa  Kilimo , Mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  akizungumza na  wakulima wa Tumbaku wilaya ya manyoni mkoa wa Singida jana
Diwani  wa kata ya Mitundu wilaya ya Manyoni Bw Andrea Madole  akimkabidhi nyalaka mbali mbali za uthibitisho wa michango kandamizi  wanayobambikizwa  wakulima wa Tumbaku na Kitengo  cha AMIS   waziri wa  kilimo ,mifugo na Uvuvi Bw Mwigulu Nchemba ambae alitangaza   kufuta michango  hiyo
Wakulima wa Tumbaku  wakitoa kero  zao kwa  waziri Nchemba (hayupo pichani)
Wabunge  wakisikiliza kero  za  wakulima wa Tumbaku
Waziri wa Mifugo na uvuvi Bw Mwigulu Nchemba  (kushoto) akimsikiliza kwa makini Mbunge wa Singida Kaskazin Bw Lazaro Nyalandu  wakati  akieleza kilio  cha wakulima wa Tumbaku  wilaya ya Manyoni wakati wa  mkutano wa  waziri Nchemba na wakulima wa Tumbaku  uliofanyika  ukumbi wa CCM Manyoni jana
…………………………………………………………………………………………….
Na MatukiodaimaBlog,Manyoni WAZIRI wa  kilimo ,mifugo na  uvuvi  Bw Mwigulu  Nchemba amefuta michango  hewa iliyokuwa ikichangiwa na wakulima wa Tumbaku  kwa  UNION kwa  kupitia  kitengo  cha AMIS huku akiagiza serikali  ya  wilaya ya Manyoni  kuwachukulia hatua  kali aofisa  ushirika mkoa  Andru Msafiri na afisa  ushirika Wilaya   hiyo Bw Alfred Sekiete iwapo watabainika  kuhusika  deni la bilioni  7  ambalo wanadaiwa benki wakulima  wa tumbaku.
 
Waziri Nchemba  alilazimika kutoa maagizo  hayo  baada  ya  wakulima  wa zao hilo la Tumbaku  kulalamikia utaratibu mbaya wa baadhi ya  viongozi wa UNION na APEX pamoja na baadhi ya maofisa  ushirika   kujinufaisha  kupitia mgongo  wa  wakulima hao.
 
Akitoa agizo  hilo  jana mjini Manyoni  wakati wa  mkutano  wa  pamoja kati yake na  wakulima wa  Tumbaku na viongozi  mbali mbali  wa Serikali  ya  wilaya ya Manyoni na wabunge  wanaotoka  wilaya ya Maeneo  yanayolimwa Tumbaku  mkoani Singida.
 
Waziri Nchemba  alisema  kuwa  baadhi  ya mambo  ambayo serikali  ya Rais Dr John Magufuli  haipendi  kuona ni  pamoja na  wakulima kubebeshwa mizigo mikubwa ambayo kimsingi haiwasaidii kupiga hatua kimaendeleo  zaidi ya  kuwatesa .
 
Alisema  inashangaza  kuona   wakulima  hao  kuendelea  kuumizwa na  viongozi  wachache ambao  wamegeuza  wakulima ni  kichaka cha  wao  kujificha  kujinufaisha  kupitia wakulima.
 
“ Mambo  ya ajabu  sana  hiki kitu  kinaitwa AMIS ni kuwatoza  wakulima michango ya ajabu ajabu  eti  wakulima  kutozwa  dola 1200 kwa  ajili  ya kusafirisha Tumbaku toka  Dar es Salaam kwenda UNION   pia  wanachangia dola 10 kwa  kutunza  kumbukumbu zao  ,dola 3 kupakia na  kushusha mara mchango kwa ajili ya ADMIN   mambo ya ajabu kabisa wakulima wanahusika  vipi na malipo maadmin yani wanatumia lugha  za  kijanja kijanja  kuwaibia  wakulima ADMIN wa makundi kama yale ya Whatsap kwa wakulima  tena…sasa kuanzia leo natangaza  kufuta michango  hii isiyo na maelezo ya kutosha na kuagiza  kujipanga upya kwa  kuwashirikisha   wakulima na taarifa  hiyo ndani ya siku 7 niipate “
 
Waziri chemba  alisema  kuwa kabla ya  kuanza  kuwatoza  wakulima hao michango ni  vizuri  makubaliano ya  michango  hiyo yafanyike  upya kwa kuwashirikisha  wakulima na sio kuendelea  kutumia taratibu  za  zamani ambazo ni mzigo kwa  mkulima.
 
Kuhusu maafisa  ushiriki  kudaiwa  kukopa  benki  kupitia mgongo wa  wakulima  wa  tumbaku na  kupelekea  wakulima hao  kudaiwa  deni  benki  la Tsh bilioni 7 aliagiza mkuu wa  wilaya ya Manyoni kuagiza wakaguzi  na wataalam wake  kufanya  uchunguzi  na iwapo itabainika  kuwa maofisa  hao  walihusika na deni  hilo  hatua  stahiki  kuchukuliwa dhidi 

0 maoni:

Chapisha Maoni