Posted by Esta Malibiche on Sept3.2016 in NEWS
Na Masanja Mabula –Pemba
JUMLA ya magunia 21 ya karafuu
kavu na makonyo yamekamatwa na askari wa operesheni ya kuzuia magendo ya
karafuu inayoendeshwa na vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
Kisiwani Pemba vikiwa tayari kusafirishwa kupelekwa nje ya nchi kwa
njia ya magendo.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu
wa Operesheni hiyo , Luteni Kanali Jabir Hamza kutoka Jeshi la Kujenga
Uchumi Zanzibar (JKU) amesema karafuu hizo zimekamatwa Shehia ya
Tondooni Wilaya ya Micheweni wakati askari wakiwa katika doria za
kawaida.
Amesema kuwa kati magunia hayo , 18 yalikuwa na karafuu kavu wakati matatu pamoja na kipeto kimoja yalikuwa na makonyo .
Luteni Jabir ameeleza kuwa
alfajiri ya Semtemba 3, mwaka huu majira ya 10:00 katika ufukwe wa
bahari ya Tondooni askari hao walizikamata karafuu pamoja na makonyo
hayo zikiwa zinasubiri maji ya yajae ili ziweze kusafirishwa.
“Alfajiri ya leo (jana) huko
Tondooni Wilaya ya Micheweni vijana wetu wakiwa katika doria
wamefanikiwa kuzima jaribio la kutaka kusafirisha karafuu hizo kwenda
nje nchi, na operesheni hii itakuwa ni endelevu” alifahamisha luteni
Jabir
Kwa upande wake Kamanda wa KMKM
Kamandi ya Pemba Khamis Taji Khamis ameeleza kuwa kikosi chake
kitazianika na kuzitenganisha karafuu kavu na makonyo na baadae
kuzipeleka Shirika la Biahara la Taifa la Zanzibar (ZSTC) kwa ajili ya
kuuzwa.
“Kwa sasa karafuu pamoja na
makonyo hayo yapo chini ya uanglizi wa kikosi cha KMKM Wete ,
tutazianika na baada ya kukauka tutazikadhiwa uongozi wa ZSTC kwa hatua
zaidi” Alifafanua Kamanda Taji.
Nae Kamanda wa Operesheni wa
kikosi cha KMKM Pemba Hussein Mohammed Seif amesema kuwa wafanyabiashara
wa magendo wamekuwa wakiikosesha Serikali mapato muhimu kwa ajili
huduma za kijamii na maendeleo .
Aidha Kamanda Hussein
amesisitiza kuwa Serikali haitokua tayari kuona biashara ya magendo
inaendelea kufanyika kwani inawanufaisha wachache , huku jamii inakosa
fedha kwa ajili ya kusaidia kupatikana huduma muhimu za kijamii ikiwemo
afya , maji barabara na elimu .
Amewataka wafanyabiashara hao
kuacha kuichafua sifa ya karafuu ya Zanzibar kwa kuzichanganya na
makonyo pindi wanapoenda kuziuzaili kulinda hadhi ya karafuu ya
Zanzibar katika masoko ya nje.
Mbali na kukamatwa kwa karafuu
hizo hakuna mtu au chombo kinachohusishwa na usafirishaji huo wa na
kuwataka wananchi kushirikiaa na vikosi kwa kutoa taarifa sahihi ambazo
zitawezesha kukamatwa kwa wanaojihusisha na vitendo vya uhujumu uchumi
kwa kusafirisha karafuu nje ya nchi.
0 maoni:
Chapisha Maoni