Wafanyakazi
wa kampuni ya simu ya Zantel leo wameshiriki katika zoezi la kupanda
miti kwenye hifadhi ya Masingini iliyopo magharibi mwa kisiwa cha
Unguja kama moja ya jitihada zake katika kutekeleza mpango wa kutunza
na kuhifadhi mazingira visiwani Zanzibar.
Eneo
la hifadhi ya msingini lipo mita 120 kutoka usawa wa bahari na ni eneo
lenye vyanzo vingi vya maji ambavyo vinakadiriwa kutoa lita 27,400,000
kwa ajili ya matumizi ya kila siku ya wakazi wa Zanzibar.
Akizungumza
wakati wa upandaji miti, Afsa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya simu ya
Zantel,bwana Benoit Janin alisema kupanda miti kutasaidia kuzuia
mmomonyoko wa ardhi, kuongeza rutuba ya udongo na pia kulinda vyanzo
vya maji.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Zantel, Benoit Janin akipanda mti katika hifadhi ya
Masingini kwa kushirikiana na Bi Nassim Said Mohameid (Kulia) na kushoto
ni Mkurugenzi wa Misitu na Maliasili zisizorejesheka wa Zanzibar bwana
Sheha Idrissa Hamdani.
‘Kama
Kampuni ya simu inayotoa huduma ya mawasiliano kwa wakazi wa visiwani
ni lazima tuhakikishe tunatunza na kuhifadhi mazingira kama moja ya
rasilimali muhimu kwa ajili ya ustawi wa jamii yetu’alisema Bw Janin.
Zoezi
hili la kupanda miti limefanyika leo, ikiwa ni wiki moja tu toka
uzinduzi wa mtandao wa 4G visiwani hapa, hatua inayoonyesha kuwa kampuni
ya Zantel imejipanga katika mpango wa kuhakikisha inalinda na kuhifadhi
mazingira kwa kushirikiana na serekali yetu .
Mkurugenzi Mtendaji wa Zantel, Benoit Janin akipanda mti katika hifadhi ya Masingini.
Akizungumza
baada ya tukio hilo, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa
Mazingira Zanzibar, bwana Sheha Mjaja Juma aliwapongeza wafanyakazi wa
kampuni ya simu ya Zantel kwa kuweza kushiriki kwenye zoezi hilo la
kutunza na kuhifadhi mazingira.
‘Madhumuni
ya zoezi hili la upandaji miti hapa Masingini yamelenga kusaidia
jitihada za kutunza na kulinda vyanzo vya maji, msitu pia kuzuia
mmonyoko wa ardhi ili kulinda viumbe hai vilivyopo kwenye eneo hilo’
alisema bwana Sheha.
Mkuu
wa Zantel kwa upande wa Zanzibar, Mohameid Mussa (katikakati) akipanda
mti kwa kushirikiana na Hamza Zuheri, Meneja wa Mtandao na Vifaa vya
mawasiliano wa Zantel (kulia) pamoja na Mkurugenzi wa Misitu na
Maliasili zisizorejesheka wa Zanzibar bwana Sheha Idrissa Hamdani
(kushoto).
Mkurugenzi
wa Masoko wa Zantel, Bi Progress Chissenga akipanda miti katika hifadhi
ya Masingini. Anayemsaidia kushoto ni Mkurugenzi wa Misitu na Maliasili
zisizorejesheka wa Zanzibar bwana Sheha Idrissa Hamdani.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Zantel, Benoit Janin akipewa maelezo kuhusu hifadhi ya
Masingini Bi Nassim Said Mohameid (Kushoto) wakati wa zoezi la upandaji
miti lilofanywa na wafanyakazi wa Zantel.
Wafanyakazi wa Zantel kutoka kushoto Deus Mtena, Winnes Lyaro na Leonard Kameta wakipanda mti katika hifadhi ya Masingini,
Mwanasheria wa Zantel Bi Julia Kilala akipanda miti kwa kushirikina na watoto wake Noah and Nathan Kilala.
Wafanyakazi
wa Zantel na wafanyakazi wa Wizara ya Kilimo na Maliasili wakiwa katika
picha ya pamoja baada ya kumaliza zoezi la upandaji miti.
0 maoni:
Chapisha Maoni