PICHA NA IKULU
Mama Maria Nyerere aliyeongozana
na Mwanae Mheshimiwa Makongoro Nyerere amesema kukamilika kwa daraja
hilo ambalo ujenzi wake umegharimu shilingi Bilioni 254.12 kumekamilisha
mpango wa miaka mingi ulioanzishwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu
Julius Kambarage Nyerere aliyekuwa na nia ya kujenga daraja katika eneo
hilo la mkondo wa bahari lakini kwa sababu ya ufinyu wa bajeti
haikuwezekana.
Aidha, Mama Maria Nyerere
amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe
Magufuli kwa kuamua Daraja hilo liitwe Daraja la Nyerere kwa heshimu ya
Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, na amebainisha
kuwa uamuzi huo utaviwezesha vizazi vijavyo kutambua juhudi zilizofanywa
na mmewe katika ujenzi wa nchi.
“Mimi ninamshukuru sana Rais
kwa maana ilikuwa lipewe jina lake, lakini yeye Mungu akamjaalia akasema
kwamba hapana tukumbuke tulikotoka, kwa hiyo najisikia vizuri sana, na
familia nayo inajisikia vizuri sana, lakini zaidi na watanzania
wanajisikia vizuri sana, kwa maana watakuwa wanaulizana Nyerere alikuwa
ni nani?” Amesisitiza Mama Maria Nyerere.
Daraja la Nyerere lenye urefu wa
meta 680, upana wa meta 32, njia sita za magari na barabara unganishi
zenye urefu wa kilometa 2.5, lilifunguliwa na Rais wa awamu ya tano Dkt.
John Pombe Magufuli tarehe 19 Aprili, 2016 na linakuwa kiunganishi
muhimu kati ya Kigamboni na katikati ya Jiji la Dar es salaam.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
27 Aprili, 2016
.
0 maoni:
Chapisha Maoni