Jumatatu, 25 Aprili 2016

NHIF YAPELEKA HUDUMA YA MADAKTARI BINGWA MKOANI NJOMBE

2
Mganga Mkuu wa  mkoa wa Njombe Dokta Samuel Mgema akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma  za madaktari bingwa mjini Njombe wanaowafanyia upasuaji na matibabu  wagonjwa mbalimbali kwa  mikoa husika, kulia ni Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Mohammed Bakari
3
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Ushauri wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Dokta Frank Lekey akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma  za madaktari bingwa mjini Njombe wanaowafanyia upasuaji na matibabu  wagonjwa mbalimbali kwa  mikoa husika,kushoto ni Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Mohammed Bakari.
5
Baadhi ya watumishi na madaktari pamoja na wananchi waliohudhuria katika uzinduzi huo.
6
Mkuu wa mkoa wa NJOMBE  Mh. Rehema  Nchimbi akiwa katika picha ya pamoja viongozi mbalimbali mara baada ya uzunduzi huo uliofanyika mjini Njombe leo.
………………………………………………………………………………………………..
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirkiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, wiki hii inaendesha zoezi la huduma za madaktari bingwa katika mikoa ya Njombe na Iringa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo mkoani Njombe Mganga Mkuu wa Serikali Profesa Mohammed Bakari amesema serikali itaendelea kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya kuhakikisha kuwa huduma hizo zinapelekwa katika maeneo mengi ambako wananchi wanahitaji huduma za madaktari  bingwa ili kukabiliana na upungufu uliopo.
Amesema pamoja na kuendelea kutumia huduma hizo za muda za madaktari Bingwa, Serikali kupitia Wizara ya Afya, itajitahidi kujenga miundo mbinu bora ya sekta ya afya na kusogeza huduma karibu zaidi na wananchi walio wengi.
Akizungumza kabla ya kumkaribisha Mganga Mkuu wa Serikali, Mganga Mkuu wa  mkoa wa Njombe Dokta Samuel Mgema, amesema hospitali yake inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na uchakavu wa majengo na ufinyu wa nafasi ikilingwanishwa na idadi kubwa ya wagonjwa wanaohudumiwa katika hospitali hiyo.
Ameomba Serikali iharakishe mchakato wa kujenga Hospitali mpya ya mkoa ili kukidhi mahitaji ya wananchi wa mkoa wa Njomba, kwani hospitali inayotumika hivi sasa ya Kibena ilikuwa na hadhi ya hospitali ya wilaya na kupandishwa hadi baada ya kutangazwa kwa mkoa mpya wa Njombe, miaka minne iliyipita.
  
Naye Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Ushauri wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Dokta Frank Lekey amesema huduma hizo za madaktari bingwa zimekuwa zikitolewa na Mfuko wake kama sehemu ya kuunga mkono juhudi za Serikali ya kupeleka huduma bora za matibabu kwa wanachama wa NHIF na kwa wananchi kwa ujumla.
Asema hadi sasa huduma hizo zimeshatolewa katika mikoa 14, ambazo zaidi ya wagonjwa 11,400 wamepatiwa huduma, miongoni mwao zaidi ya wagonjwa 340 walifanyiwa upasuaji wa kitaalamu.
Amesisitiza kuwa huduma hizo zinatolewa kwa wananchi wote bila ubaguzi kwa kufuata taratibu za kawaida za malipo za hospitali husika.

0 maoni:

Chapisha Maoni