Ijumaa, 22 Aprili 2016

Aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo la Micheweni (CUF) kufikishwa mahakamani kwa shambulio

58741041
Na Masanja Mabula –Pemba 
JESHI la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba limeagiza kukamatwa  na kufikishwa mahamakani aliyekuwa , Mwakilishi wa Jimbo la Micheweni (CUF) kwa mihula miwili (2005-2015)  Subeti Khamis Faki anayetuhumiwa kutenda kosa la shambulio  la kuumiza mwili .
Kamandawa Polisi Mkoa  wa Kaskazini Pemba , Kamishina Msaidizi Mwandamizi Hassan Nassir Ali akizungumza na mwananachi Ofisini jana ,  alisema kwamba Subeti anatuhumiwa kumshambulia kwa kumpiga magongo Mbwana Nassor Shilingi (30) na kumsababishia maumivu mwilini .
Alisema kuwa tukio hilo limetokea jana (juzi) aprili 20 majira ya saa 2:15 asubuhi huko Shehia ya Mjini Wingwi Wilaya ya Micheweni baada ya kutokea hali ya kutoelewana kati ya pande hizo mbili .
Kamanda Hassan Nassir Ali alizidi kufahamisha kwamba siku ya tukio huko Mjini Wingwi Subeti alimwita mbwa , kijana huyo wakati akimzuia kuchota maji kwenye bomba ya maji  nyumbani kwa Mbwana  Nassor Shilingi.
“Nimemwagiza OCD Wilaya ya Micheweni amkamate na kumfikisha mahakamani aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo la Micheweni , Subeti Khamis Faki kutokana na kutenda kosa la shambulio ya kuumiza mwili ”alifahamisha .
Aidha taarifa zaidi zinasema kwamba ugomvi umetokea wakati Subeti akijaribu kumzuia jirani yake kutotumia bomba ya maji inayomilikiwa na ndg Mbwana akidai kwamba vitu vya wanachama wa CCM wamegoma kuvitumia .
Hata hivyo kamanda Nassir akikataa kulihusisha tukio hilo na masuala ya kisiasa kwani alisema kwamba ni ugomvi wa watu binafsi .
Akizungumza na mwananchi mjeruhiwa wa tukio hilo alisema kuwa chanzo chake kimesababishwa na mgeni aliyekuja katika mtaa wao , ambapo alikwenda kwenye bomba ya maji kwa ajili ya kufua nguo zake na ndipo Subeti alimwambia asitumie vitu vya mbwa kwani wamevigomea .
Alieleza kwamba baada ya maneno hayo , mjeruhiwa katika tukio hilo alipinga kuitwa mbwa na wakati akiondoka kwenye bomba hiyo alijikuta akipigwa magongo sehemu za mgongoni na kupata maumivu .
“Unajua alikuja mgeni hapa mtaani petu , sijui kama ni CCM au CUF akaanza kufua nguo katika bomba ya maji , lakini cha kushangaza Subeti alimkataza kutumia bomba hii akisema ni ya mbwa  na sisi tumewagomea ”alieleza Mbwana .
Baada ya kutokea kwa tukio hilo , mtuhumiwa huyo alipotafutwa na mwandishi wa habari hizi  kuzungumzia tuhuma hizo alidai kutokuwa tayari kuzungumza na vyombo vya habari kwa wakati ule .
Kumekuwako na matukio ya kushambuliana mara kwa mara katika shehia ya Mjini Wingwi baada ya kufanyika uchaguzi Mkuu wa marejeo hapo machi 20 uliokipa ushind chama cha CCM .
Awali tukio kama hilo lilitokea baada ya Tume ya Uhaguzi kutangaza  matokeo ya uchaguzi huo ambapo fujo zilotokea na kusababisha askari kutumia mabomu ya kutoa machozi kuwatuliza wafuasi wa vyma vya CCM na CUF walikuwa wakishambuliana .

0 maoni:

Chapisha Maoni