Jumatano, 27 Aprili 2016

DR.NDALICHAKO AWAASA WALIMU KUACHA UTORO KATIKA VITUO VYAO VYA KAZI





Waziri wa Elimu na Mfunzo ya Ufundi Dr Joyce Ndalichako  amewataka wadhibiti ubora wa Elimu nchini  kuhakikisha wanatoa tarifa za utoro wa walimu katika ngazi za juu  iili wizara husika iweze kuwachukulia hatua
Waziri Ndalichako aliitoa kauli hiyo jana wakati alifungua mafunzo kwa wakaguzi wa uhakiki ubora wa elimu Tanzania yaliyo fanyika katika chuo cha walimu Kleruu mkoani hapa yaliojumuisha mikoa sita ya nyanda za juu kusini ambayo  Iringa, Njombe, Ruvuma, Katavi, Sumbawanga, Songwe na Mbeya. Mafunzo hayo yana husu uhakiki wa ubora wa KKK (Kusoma, Kuandika na Kuhesabu).
 Akifungua mafunzo hayo Dr Ndalichako alisema serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wake Dr.John Magufuli  imepania kukuza ubora wa elimu inayo tolewa  hapa nchini hivyo  lazima  iboreshwaili kiwango cha ufauru kiweze kuongezeka
Kumekuwa na changamoto kubwa mashuleni  katika usahihihi  wa takwimu  kutokana na uzembe wa baadhi ya wathibiti kutoa taarifa za uongo  kuhusu idadi ya walimu wanaohudhuria vipindi kufundisha pamoja na wanafunzi wanaohudhuria masomo
Ndalichako alisema wakaguzi wanapaswa kuhakiki mitaala inayotolewa kama inafundishwa ipasavyo pamoja na kukagua mahudhurio ya walimu na wananfunzi ili kupata uwiano na pale inapobainika kuwa kuna mapungufu taarifa itolewe mapema ili kuweza kutatua tatizo kabla  ya athali haijatokea.
Tumeshuhudia  idadi kubwa ya wafanyakazi hewa nchini na sekta ya inayooongoza ni hii ya Elimu,hivyo hatuna budi kuwa waangalifu katika utumishi wetu kutokanan na dhamana tuliyopewa na kiongozi wetu.Sitamfumbia macho kiongozi yeyote katika sekta yangu atakaeleta uzembe kazini  nitapambana nae <<<alisema
Alisema swala la uwiano baina ya walimu na wanafunzi ni muhimu sana ili wanafunzi waweze kufundishwa vzuri na hatimae waweze kufauhuru kwa kiwango cha hali ya juu.
Alisema eneo  lingine ambalo mkaguzi anapaswa kufanya pale anapokuwa anafanya ukaguzi shuleni anatakiwa kuangalia ubora wa vitabu vinavyotumikapamoja na vifaa vyote ni lazima viowe na ubora unaosadikiwa kufuata mitaala.
Aidhaaliwataka maafisa Elimu kkuendelea kutoa Elimu kwa wazazi na walezi kuhusu utoaji wa Elimu bila malipo kutokanan na baadhi ya wazazi kutokuwa na uelewa wa kutosha kwa kufukiri michango yote imesitishwa hata wanashindwa kuwanunulia watoto wao mahitaji muhimu ya shule kama sale na daftari wakitegemea serikali huku wakifikiri serikali ndiyo yenye mamlaka.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa  wa Iringa Amina Masenza  alimuomba waziri kuhakiksha Wahakiki ubora wanapewa kipaumbele katika kukuza elimu Tanzania kwa kuboreshewa maslai yao ili waweze kufanya kazi kwa ufanisi
Masenza alisema kuwa wakati serikali inaendelea kuboresha masalahi ya walimu izingatie sana katika kuhakikisha nyumba na malimbikizo ya madai yao yanatatuliwa haraka iwezekananyo.Na alimuomba waziri Ndalichako ku;lisimamia na kuhakikissha linapewa kipaumbele

Naye Mkuu wa wilaya bwana Richard Kasesela akitoa salamu alisema wakati muafaka umefika wa  kubadili KKK iliyopo iliyozoeleka sasa yaani KULA, KULALA na KUCHEZA kuiirejesha kwenye maana halisi ya KUSOMA, KUANDIKA na KUHESABU kutokana na baadhi ya wanafunzi kuhitimu elimu ya msingi bila kujua kusoma na kuandika.
Alisema hali hii inatokana na walimu kutofuatilia maendeleo ya mwanafunzi mmoja mmoja pamoja na wazazi kutokuwa makini na watoto wao kwa kukagua daftari na kutofuatilia masomo yao,na hatimae kuwaachia walimu pekee.

0 maoni:

Chapisha Maoni