Jumapili, 24 Aprili 2016

Juliana Shonza asema amejipanga vilivyo kuwakwamua wanawake kiuchumi mkoani Songwe



shon5

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza, akiwa amebebwa na Wanawake, Wajumbe wa Baraza la Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Wilaya ya Momba mkoani hapa jana alipokutana nao mjini Tunduma kwa lengo la kuwashukuru kwa kumchagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Picha na Mpigapicha Wetu
shon6
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza, akizungumza na wanawake, Wajumbe wa Baraza la Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Wilaya ya Momba Mkoa wa Songwe, jana alipokutana nao mjini Tunduma kwa lengo la kuwashukuru kwa kumchagua kwake katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Picha na Mpigapicha Wetu
shon1
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Rose Tweve (kulia)  akimsisitiza jambo Mbunge mwenzie wa Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza jana wakati Shonza alipokutana na Wajumbe wa Baraza la Wanawake wa CCM (UWT)  Wilaya ya Momba   mjini Tunduma kwa lengo la kuwashukuru wajumbe hao kwa kumchagua kuwa mbunge wa viti maalum mkoani hapa katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana. Picha na Mpigapicha Wetu.
shon3
Mbunge wa  Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, Juliana Sonza na Mbunge mwenzia wa Mkoa wa Iringa, Rose  Tweve ( wa tatu kushoto) wakiserebuka na wajumbe wa Baraza la Wanawake wa CCM Wilaya ya Momba (UWT)  Mkoa wa Songwe, jana walipokutana nao mjini Tunduma kwa lengo la kuwashukuru  kwa kumchagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana kupitia UWT. Picha na Mpigapicha Wetu.
shon4Mbunge wa  Viti Maalum, Mkoa wa Songwe, Juliana Sonza (aliyeshika kipaza sauti) na Mbunge mwenzia wa Mkoa wa Iringa, Rose  Tweve ( wa tatu kushoto) wakiserebuka na wajumbe wa Baraza la Wanawake wa CCM Wilaya ya Momba (UWT)  Mkoa wa Songwe, jana walipokutana nao mjini Tunduma kwa lengo la kuwashukuru  kwa kumchagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana kupitia UWT. Picha na Mpigapicha Wetu.
…………………………………………………………………………………………………..
Na Mwandishi Wetu
Tunduma. Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Songwe, Juliana Shonza amesema amejipanga vilivyo kuhakikisha anawainua wanawake wa mkoa  huo, kiuchumi kwa kuwazesha kufanya ujasiriamali utakaowaingizia kipato.
Shonza alitoa kauli hiyo jana  kwa  wajumbe wa Baraza la Wawanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT) Wilaya ya Momba, alipokutana nao mjini Tunduma kwa lengo la kuwashukuru kwa kumchagua katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Shonza ambaye aliongozana na Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Rose Tweve, alisema  katika kuhakikisha adhima yake  ya kuwanua wanawake hao inatimia ameanzisha mfuko maalumu alioita ‘Songwe Women Foundation”   utakaolenga kuwasaidia wanawake wa umoja huo.
“Ninawaombeni sana undeni vikundi, hakikisheni mnavisajili na fedha ya kusajili vikundi vyenu nitatoa mimi, na nimeanzia mfuko maalum kwa ajili ya wanawake wote wa mkoa wa Songwe, na nimeweka Sh 20 milioni na kila kikundi kwenye kata zenu mtapewa Sh200,000 kwa ajili ya kuanzisha  mradi mtakaona unafaa. Niliwaahidi kuwainua nitafanye mtakavyotaka nyinyi.
Kupitia mfuko huo, nitataka mniambie ni mradi gani mnataka kuufanya. Lakini mbali na kuwawezesha kifedha lakini kabla ya kuanza kuanzisha mradi huo kwanza nitawaletea wataalamu wa masomo ya ujasiriamali watawafundisha ili iwasaidie kuendesha mradi wenu,” alisema Shonza.
Alisema kupitia mfuko huo, tayari ameanza kuzungumza na wadau mbalimbali watakaomsadia kuwawezesha wanawake wa mkoa wake kujikwamua kiuchumi huku akiwasisitizia kuchapa kazi bila kuchoka wala kubweteka kwa vile wanapata msaada kutoka kwake.
Kwa upande wake, Mbunge wa Iringa, Tweve aliyemsindikiza Shonza kuzungumza na wanawake hao, aliwataka wanawake wa Songwe kujivunia mbunge wao (Shonza) kwani ni mchapa kazi na ni mtu mwenye mtandao npana ambao utawawezesha  kujikwamua kiuchumi.
“kwanza ninawashukuru sana wanawake wa Momba, na Songwe kwa ujumla kumuamini motto wenu huyu Shonza, ni muda mfupi nimefahamiana naye. Na hii ni kutokana na uchapa kazi wake, ninaombe mtumieni vyema bila kusahau na nyinyi kufanya kazi bila kuchoka.” Alisema Tweve.
Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Momba, Isavera Mwanisenga alisema CCM katika uchaguzi uliopita walipoteza majimbo yote mawili ya Momba na Tunduma hivyo lakini bado hawajafa moyo kwani bado wanaye mbunge Shonza anawapigania huku wakiendelea kujipanga kurudisha majimbo hayo kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

0 maoni:

Chapisha Maoni