Alhamisi, 28 Aprili 2016

SERIKALI KUPITIA WIZARA YA ELIMU YATOA AGIZO KWA MKURUGENZI IRINGA DC





Serikali kupitia wizara ya Elimu na mafunzo ya ufundi imetoa agizo kwa mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa vijijini kuhakikisha wanafanya ukarabati  wavyumba vya maabala katika shule ya sekondari Tosamaganga kutokana na uchakavu uliopo.
Maabala hayo yamedumu kwa muda mrefu  bila kufanyiwa marekebisho  na kuakaratiwa hali inayopelekea  mabomba ya maji yaliyopo ndani ya vyumba hivyo kutofanya kazi  na  kusababisha ugumu wa wananfunzi kujifunza kwa vitendo .
Agizo hilo limetolewa na waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi Dkt Joyce Ndalichako wakati wa ziara yake al;iyoifanya mkoani hapa juzi  na kutembelea shule hiyo kongwe iliyodumu kwa muda wa  miaka 89 toka ilipoanza mwa 1926 .
Ndalichako alimtaka mgurugenzi na Halmashauri ya Iringa kwa ujumla  wasimamie na wahakikishe wanaboresha vifaa vyote  vya maabala vilivyochakaa ili wanafunzi waweze kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu sayansi.
.”””””””””””””Tosamaganga ni shule ambayo tunatakiwa tujivunie watanzania  na inahistoria ndani tan chi na Taifa kwa ujumla.Viongozi wengi waliowahai kushika nyadhifa mbalimbali nchininn wamesoma katika shule hii,hivyo hatuna budi kuienzi na kuitunza ili ionekana kuwa ni shule bora hapa nchini  lazima iwe na vifaa vya kujifunzia….alisema
Aidha Dkt Ndalichako alizungumza na walimu wanaofundisha katika shule hiyo na kutoa maagizo kwa kusema kuwa  walimu ni wito,hivyo hawana budi kutumia muda wao mwingi kufundisha kwa bidii ili kiwango cha ufauru kiweze kuongezeka.
Pia alohoji kuhusiana na kushuka kwa kiwango cha ufahuru kwa wananfunzi katika shule hiyo hivi sasa ukilinganisha na hapo awali,ambapo shule hiyo pamoja na ukongwe lakini imeshindwa kuingia kwenye kumi bora katika matokeo ya mitihanai ya kidato cha nne na sita.
“””’’’’’’’’’’’’’Hii hali haivumiliki kabisa walimu fanyeni kazi mliyoajiliwa na serikali ili Tosamaganga  iendelee kutoa viongozi bora na siyo bora viongozi kutokana na historia yake’’’’’alisema
Alisema wakati serikali inaendelea kushughulikia madai yao yasiyo ya kimshahara aliwataka kuwa na moyo wa uzalendo kufundisha bila kuchoka ili kiwango cha ufahuru kiweze kuongezeka.
Kwa upande wake mkuu wa shule hiyo Dismas Mgimwa alimshukuru waziri wa Elimu kwa kuitembelea shule hiyo na kubaini changamoto zinazoikabili shule na kuahidi kuzishughulikia kwa kuzitatua.
Mgimwa alisema swala la uakarabati wa vyumba vya maabala ni kilio cha muda mrefu lakinin imeshangwazwa kuonekana halifanyiwi kazi hali inayopelekea wanafunzi kushindwa kutumia ipasavyo vyumba hivyo.
Alisema Pamoja na uchakavu wa vifaa na vyumba vya maabala lakini shule ya Tosamaganga inakabiliwa na uhaba wa walimu wa sayansina kuseama  kuwa ni wachache ukilinganisha na uhitaji wa wanafunzi,hivyo serikali inatakiwa kuangalia kwa jicho pevu ili kutatua changamoto hiyo na kuleta uwiano sawa na wanafunzi.


Walimu  nao walitoa kilio na malalmiko yao kwa waziri Ndalichako, ambapo mwalimu Koleta Mfugale  aliiomba serikali iangalia kwa jicho pevu swala la uhaba wa nyumba za walimu na kusema kuwa kutokanan na changamoto hiyo, wengi wao wanakaa nje ya shule  zaidi ya km kadha hivyo kushindwa kuleta ufanisi katika kazi.
Mfugale aliitaka serikalai kutoa tamkoa rasmi la kitaifa kukataza matumizi ya simu kwa wanafunzi hasa katika shule za sekondari za kutwa na bweni kutokana na wanafunzi waliowengi kumiliki simu na  kupoteza muda mwingi katika matumizi ya simu za kuliko kujifunza hali inayochangia kushuka kwa kiwango cha ufahurukatika shule hiyo.
.



0 maoni:

Chapisha Maoni