Ijumaa, 22 Aprili 2016

MAKATIBU WAKUU HABARI, UTALII, UTAMADUNI NA MICHEZO ZANZIBAR WAKABIDHIANA OFISI


DSC_1814
Katibu Mkuu Wizara ya Habari Utalii Utamaduni na Michezo Omar Hassan Omar kushoto akikabithiwa nyaraka na Katibu Mkuu Mstaafu Ali Mwinyikai katika makabidhiano yaliyofanyika katika ukumbi  wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Mnazi Mmoja Zanzibar .
…………………………………………………………………………………………………
Mwashungi Tahir Maelezo Zanzibar 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo Omar Hassan Omar amesema azma ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar ni kuwapatia wafanyakazi wake  huduma  bora ili waweza kundeleza kazi zao kwa ufanisi.
Hayo ameyasema leo huko katika ukumbi wa Wizara   Mnazi mmoja baada ya kukabidhiwa  Ofisi na Katibu Mkuu aliemaliza muda wake Ali Mwinyikai .
Amesema utendaji  kazi wa Serikali ni wapamoja   na sio mtu mmoja mmoja hivyo aliwaomba viongozi na wafanyakazi wa wizara kumpa mashirikiano makubwa katika utendaji wa majukumu yake.
Katibu Mkuu alisema Wizara  ipo katika hali nzuri kiutendaji  hivi sasa na  ameahidi  kufanyakazi kwa juhudi kuweza kupata ufanisi zaidi na  kuleta maendeleo.
Amesema yuko tayari kupokea ushauri  na   kukosolewa  na wafanyakazi wenzake na amewahakikishia kwamba watashirikiana ili waweze kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali katika Wizara hiyo.
“Sisi viongozi peke yetu hatuwezi kufika mbali katika kuleta maendeleo bila ya mashirikiano ya pamoja  hivyo mashirikiano ya pamoja ndio mafanikio yetu sote,” alisema Katibu Mkuu.
Ameahidi kusimamia na kudhibiti matumizi  ya  fedha ya Wizara ili  kuongeza mapato na kuimarisha Idara , Taasisi na  kuboresha maslahi hasa ya  taaluma kwa wafanyakazi .
Amesema Wizara ni kubwa na  imebeba taasisi muhimu katika maendeleo ya ikiwemo habari, utalii ambao ni tegemeo kubwa kwa taaifa kwa sasa, utamaduni na michezo pia ni kielelezo muhimu cha Taifa.
 Nae Katibu Mkuu mstaafu Ali Mwinyikai  amemuhakikishia Katibu Mkuu mpya kuwa yupo tayari kumpa mashirikiano ya kila hali ili  kazi  za Wizara ziende kwa kasi zaidi.
Pia aliwashukuru viongozi wenzake  wa Wizara kwa kumpa mashirikiano mazuri katika utendaji  wa kazi zake  na aliwaomba kumpa  mashirikiyano  katibu wao Mkuu wa sasa ili aweze kufanya kazi zake kwa ufanisi.
Kwa upande wake,  Naibu Katibu Mkuu mstaafu Issa Mlinngoti  akimkabidhi Naibu katibu mkuu mpya Amina Ameir Issa Ofisi amesifu mashirikiano aliyoyapata kutoka kwa wafanyakazi wenzake na kuwaomba waendelee   kumpa mashirikiano Naibu mpya ili kazi zake ziende vizuri.

0 maoni:

Chapisha Maoni