Ijumaa, 22 Aprili 2016

NEC YAPONGEZWA KWA KUSIMAMIA UCHAGUZI MKUU 2015

NRA
Na Beatrice Lyimo – MAELEZO
 Dar es Salaam
……………………………………………………………………..
Wadau mbalimbali kutoka vyama vya Siasa vilivyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba 25, 2015 wameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuendesha zoezi hilo kwa Uwazi, Haki, Amani na kwa kuzingatia Sheria na Kanuni.
Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Chama cha NRA Bw. Hassan Kasabya alipokuwa akitoa pongezi kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kutoa vyeti vya shukrani kwa washiriki hao katika huo kwa vyama vya siasa na wadau wengine.
Bw. Kasabya amesema kuwa Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliona umuhimu wa vyama hivyo kama wadau wa uchaguzi na chaguzi zote hapa nchini na kuamua kutoa kutoa vyeti vya shukrani kwa kufanikisha uchaguzi huo.
“Vyeti hivi ni kielelezo tosha cha umakini wa Tume yetu na jinsi gani wamejali na kuthamini ushiriki wa vyama vyetu, kwani pasipo vyama vyetu hivi uchaguzi mkuu hauwezi kufanyika” ameongeza Katibu  Mkuu huyo.
Aidha, kwa upande wake Katibu Mkuu kutoka Chama cha AFP Rashid Rai ametoa wito kwa Serikali kuzidi kuiwezesha Tume ya Taifa ya Uchaguzi hususan uboreshwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na kuzidi kutoa elimu ya uraia kwa wapiga kura.
Mbali na hayo, Wadau hao wameipongeza Tume hiyo kwa mabadiliko makubwa ya kiutendaji yaliyofanyika katika uchaguzi mkuu uliopita kulinganisha uchaguzi wa mwaka 2010, 2005, 2000 na 1995.
Wadau walioshiriki kuipongeza NEC kufanikisha Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana ni pamoja na Chama cha National Alliance and Reconstruction (NRA), Chama cha Alliance for Tanzania Farmers (AFP), Chama cha United Peoples Democratic Party (UPDP), Chama cha UMD, Chama cha Demokrasia Makini (MAKINI) na Chama cha Haki na Ustawi (CHAUSTA).

0 maoni:

Chapisha Maoni