Ijumaa, 29 Aprili 2016

UONGOZI WA WANAFUNZI WA CHUO CHA UONGOZI WA FEDHA ZANZIBAR (ZIFASO) WACHAGUA VIONGOZI WAPYA.

z1Wagombea  wa nafasi  ya Rais wa ZIFASO Juma Shirazi Hassan a Makamu wake Zuwena Jaku Hassan (wa katikati) wakiongozwa kuingia katika kampasi ya Chuo cha Uongozi wa Fedha Zanzibar kiliopo Chwaka Mkoa Kusini Unguja tayari kwa ajili ya kupiga kura.
z2Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi  ya wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Fedha Zanzibar Sabrina Yussuf Shaaban akielezea juu ya utaratibu mzima wa kupiga kura ili kupata viongozi wapya wa ZIFASO .
z3Mlezi wa wanafunzi wa Chuo cha Uongozi wa Fedha Zanzibar Maalim Wazir Hamad akitoa nasaha  zake kwa wapiga kura ambao ni wanafunzi wote wa chuo hicho.
z4Mgeni rasmi katika uchaguzi huo ambae ni Afisa kutoka Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) Mohd Ali Abdalla akiwanasihi  wasimamizi na wapiga kura kuendesha uchaguzi katika misingi ya haki.
z5Mgombea  pekee wa nafasi ya Rais wa ZIFASO  Juma Shirazi Hassan akipiga kura yake  katika uchaguzi huo uliofanyika chuoni Chwaka Mkoa Kusini Unguja.
z6Wasimamizi wa uchaguzi wakiwa pamoja na mawakala wa wagombea wakihesabu kura mara baada ya kukamilika zoezi la upigaji kura.
z7Mawakala na wasimamizi wa uchaguzi wakijumuisha kura ili kujua mshindi katika uchaguzi huo.
z8Rais mpya wa ZIFASO na Makamu wake Juma Shirazi Hassan na Makamu wake Zuwena Jaku Hassan wakitoa shukrani na nasaha zao  baada ya kuchaguliwa kuongoza Jumuia hiyo kwa mwaka

0 maoni:

Chapisha Maoni