Ijumaa, 29 Aprili 2016

MKUU WA WILAYA IRINGA RICHARD KASESELA aAITAKA JAMII KUWA NA NIDHAMU MAHALI PA KAZI ILI KULETA UFANISI

Mkuu wa wilaya Iringa Richard Ksesela akizungumza nawashiriki wa   mfunzo ya PUBLIC PRIVATE DIALOGUE (PPD) pamoja na kugawa vyeti kwa washiriki hao.








Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Iringa Stephen Muhapa akipokea baada ya kuhiotimu mafunzo



Mkuu wa wilaya Iringa Richard Ksesela ashiriki kufunga  mfunzo ya PUBLIC PRIVATE DIALOGUE (PPD) pamoja na kugawa vyeti kwa washiriki.

Mafunzo hayo yanaendeshwa  na Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam- Shule ya Boiashara (UDBS) na kudhaminiwa na mradi wa BEST-PPD.

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo yaliyofanyika mkoani Iringa na  kufungwa leo hii[jana]yaliyohudhuliwa na wilaya za Njombe,Iringa,Kilolo na Mufindi alisisitiza kudumisha nidhamu katika kazi  ili kuleta ufanisi mahali pa kazi,hasa katika sekta binafsi.
 Katika hotuba yake Mkuu wa Wilaya ya Iringa Richard kasesela aliyoitoa wakati akifunga, aliwataka washiriki kuyafanyia kazi yale waliyoyapata ili kuleta chachu ya maendeleo katika wilaya wanazotoka, jamii,na Taifa kwa ujumla.

Kasesela alisema mafunzo yaliyotolewa ni muhimu sana kwa Taifa letu na yana lengo la kuhimiza mijadala na mazungumzo kati ya sekta binafsi na serikali kwa ujumla.


Katika hotuba yake alisisitiza sana suala la nidhamu, na kusema kuwa nidhamu ndiyo msingi wa kujenga sekta binafsi iliyo imara. Pia aliwaasa kupunguza utitili wa jumuiya za sekta bianfsini muhimu zikaungana na kujenga moja yenye nguvu kwa maendeleo ya Taifa.

Aidha alitoa ushauri kwa halmashauri zote  nchini kufungua dawati kwa ajili ya mijadala na sekta binafsi ili ziweze kutekeleza majukumu mengine kwa niaba ya serikali.

‘’’’’’’’’’’’’’’’’Bila sekta binafsi imara uchumi wa nchi hauwezi kukua, ni muhimu sekta binafsi ikaanza kuchukua nafasi stahiki ikiwemo kutekeleza majukumu mengine kwa niaba ya serikali mfano ukuaji wa michezo mabayo inahitaji uwekezaji ili serikali iondokane na kuwekeza, nchi kama Marekani hazina wizara ya michezo" alisema.







0 maoni:

Chapisha Maoni