Ijumaa, 22 Aprili 2016

Viongozi TFF wafanya ziara TBL Group

Rais wa Shirikisho la Soka Nchini  (TFF) Jamal Malinzi akiongoza ujumbe wa maofisa wengine wawili wa shirikisho hilo wamefanya ziara makao makuu ya ofisi za TBL Group zilizopo Masaki jijini ambapo walikutana na mkurugenzi wake Mkuu Roberto Jarrin  na kufanya naye mazungumzo.
Ziara hiyo imeelezwa kuwa ina lengo la kudumisha uhusiano miongoni mwa taasisi hizo mbili hususani katika kuendeleza mchezo wa soka nchini.
msi1
Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Jamal Malinzi (wa pili kulia ) Katibu Mkuu  shirikisho hilo,  Mwesigwa Selestine (kushoto) na Mjumbe wa Kamati ya TFF Richard Sinamtwa (katikati) wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group Roberto Jarrin (Kulia ) wakati walipofanya ziara ya kikazi ofisini kwake Masaki  jijini Dar es Salaam.
msi2
msi3
Mkurugenzi Mkuu wa TBL GROUP  Roberto Jarrin (wapili kushoto)  Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Jamal Malinzi (wa pili kutoka kulia) Katibu Mkuu  shirikisho hilo , Mwesigwa Selestine  (kulia) na Mjumbe wa Kamati ya TFF, Richard Sinamtwa (kushoto )wakiwa kwenye picha ya pamoja  wakati walipotembelea katika ofisi za TBL Masaki  jijini Dar es Salaam
msi4
Mkurugenzi Mkuu wa TBL GROUP  Roberto Jarrin (katikati akisalimiana na Mjumbe wa Kamati ya TFF, Richard Sinamtwa ,  Kulia ni Rais wa shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) Jamal Malinzi

0 maoni:

Chapisha Maoni