Jumatatu, 18 Aprili 2016

MBUNGE WA MUFINDI KUSINI MENDRAD KIGOLA AANZA KUBORESHA VITUO VYA AFYA JIMBONI KWAKE




Mbunge wa Jimbo la Mufindi kusini Mhe, Mendrad Kigola ameanza kuchukua hatua za kupambana na tatizo la vifo vya Wajawazito na Watoto wachanga kwa kuboresha baadhi ya vitio vya afya katika jimbo lake.

Kigola aliyasema hayo jana wakati akizungumza na mwandishi wa mtandao huu wa Kali ya habari  kuhusu utekelezaji wa majukumu yake kutokana na vifo vya wajawazito na watoto wachanga vinavyotokana na uzazi.
‘’Mimi nimeshaanza hatua zakupambana  na tatizo hili na tayari nimeboresha vituo saba vya afya katika jimbo langu kikiwemo kituo cha afya nyololo na Malangali
.
“Lakini kuboresha zahanati na vituo vya afya pekee haitoshi ila inatakiwa kuboresha miundombinu, umeme na maji huko vijijini ndipo afya inakuwa imekamilika. Nitaishawishi serikali ihakikishe fedha inatolewa kwa ajili ya maendeleo hayo” alisema Kigola

Alisema katika Bunge lijalo la bajeti atahakikisha anasimamia Wizara ya afya ili kuhakikisha fedha inayo tengwa inaelekezwa kwenye ujenzi wa zahanati na vituo vya afya kama njia moja wapo ya kutatua tatizo hilo katika jimbo lake na Tanzania nzima kwa ujumla

Mhe, Kigola alisema katika mikakati yake ataishauri Serikali kuboresha Zahanati na vituo vya afya ili ifikapo mwaka 2025 tatizo la vifo vinavyotokana na uzazi liwe limepungua kama si kuisha kabisa

“Suala kubwa ni kuihamasisha serikali kuboresha vituo vya afya na zahanati kwa kuhakikisha kunakuwa na wataalam na dawa katika vituo hivyo ili akina mama wasipate shida pale unapofika wakati wao wa kujifungua” alisema

Hata hivyo alisema  kuboresha zahanati na vituo vya afya pekee haitoshi atahakikisha pia Serikali inaboresha miundombinu na kupeleka umeme na maji huko vijijini ili kurahisisha kazi ya utoaji wa huduma ya afya

Aidha alisema serikali inapaswa kuliona tatizo hili kama ni suala la muhimu na kuchukua hatua kwani ukitokea uzembe na kuchukuliwa mzaha tatizo linaweza kuwa kubwa zaidi na likasababisha hasara kubwa kwa Taifa.

Alisema watu wanapoongezeka bajeti pia huongezeka na kwamba serikali inatakiwa kuwa na bajeti ya kutosha ili kukidhi ongezeko la watu linalojitokeza

Hii ni kutokaa na kuonesha kuwa Tanzania ina watu milioni 45, watu milioni moja huongezeka kila mwaka ambapo inakadiliwa ongezeko la watu litakuwa mara tatu zaidi kila mwaka na kufikia watu milioni 130 ifikapo mwaka 2050

Hata hivyo alisema wananchi wanatakiwa kupanga uzazi katika uwiano mzuri ili kuwa na watoto wenye afya kuliko kubananisha watoto wasio kuwa na afya hali ambayo humuathiri hata mzazi.

“Tunapozungumzia uzazi wa mpango, ni suala pana kwa sababu kila mtu ana hoja yake lakini cha msingi ni kwamba, tunaposema watu watumie uzazi wa mpango tunamaanisha kuwa watu wazae watoto wenye interval (uwiano) mzuri kwa sababu kuna watu kila mwaka anataka kuwa na mtoto sasa hiyo haifai, Tunataka watoto wapishane vizuri kiafya wasibanane mno” alisema

0 maoni:

Chapisha Maoni