Jumatano, 27 Aprili 2016

Waajiri Wote Wanaodaiwa Malimbikizo Ya Michango Ya NSSF watakiwa Kulipa Michango Kabla Ya Tarehe 30.06.2016


1Bw. James Oigo Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji Shirika la Taifa la  Hifadhi ya Jamii NSSF akizungumza na waandhishi wa habari katika makao makuu ya shirika hilo jengo la Benjamin Mkapa wakati akielezea kuhusu waajiri wanaodaiwa madeni sugu ya michango ya wafanyakazi wao na kutamka kwamba wasipolipa michango hiyo mpaka ifikapo Juni 30 mwaka huu shirika hilo linawapeleka mahakamani, kulia ni mmoja wa maofisa waandamizi wa shirika hilo Bw. Salim Khalifan pamoja na maofisa wengine wa shirika hilo waliohudhuria katika mkutano huo.
2Baadhi ya maofisa wa shirika hilo wakiwa katika mkutano huo.
_MG_5980Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa hiyo wakati Bw James Oigo Kaimu Mkurugenzi wa Uendeshaji Shirika la Taifa la  Hifadhi ya Jamii NSSF akizungumza nao katika mkutano huo.
………………………………………………………………………………………………………………………
Shirika la Taifa la Hifadhi ya jamii (NSSF) linapenda kutoa wito kwa waajiri wote wanaodaiwa malimbikizo ya michango ya wafanyakazi wao kulipa malimbikizo hayo kabla ya tarehe 30.06.2016.
Waajiri ni moja kati ya wadau  wakubwa wa shirika letu la NSSF kwa mujibu wa kifungu cha 11(6) na 12 (1) cha sheria ya NSSF, waajiriwa wana majukumu makubwa mawili.
  1. Kuhakikisha wafanyakazi wao wanaandikishwa katika shirika la taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) mara tu wanapoajiriwa.
  1. Kuwakata michango yao asilimia 5% au 10% kutoka kwenye mshahara wa mwezi na kuwasilisha mchango huo ukiwa ni asilimia 20% ya mshahara wa mwezi, maana yake ni kwamba mwajiri baada ya kufanya makato kutoka katika mshahara wa mfanyakazi wake, anatakiwa kuongeza asilimia 10% au 15% ili ifikie asilimia 20% na kuwasilisha kwenye shirika.
Kwa mujibu wa kifungu cha 14 cha sheria ya NSSF no 28 ya mwaka 1997, waajiri wote wanatakiwa wawasilishe michango ya wafanyakazi wao ndani ya siku 30 toka tarehe ya mwisho wa mwezi husika, kwa mfano mchango wa mwezi machi,2016 , unatakiwa uwe umewasilishwa kwenye shirika kabla ya tarehe 30/4/2016 kinyume na hapo ni ukiukwaji wa sheria na ni kosa la jinai.
Lakini kuna baadhi ya waajiri kwa sababu wanazozijua wenyewe, wanashindwa kutekeleza hitaji hili la kisheria kikamilifu kwa kushindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.
Kitendo cha kutowasilisha michango ya wafanyakazi wao  kwa wakati si tu kwamba ni kosa la jinai kwa mujibu wa kifungu cha 72 (d) cha sheria ya NSSF na ambayo adhabu yake ni pamoja na kifungo cha miaka 2 jela, lakini pia ucheleweshaji huu unasababisha madhara makubwa kwa wanachama na shirika kwa ujumla.
Kutowasilisha michango kwa wakati husababisha usumbufu mkubwa kwa wanachama pale wanapostaafu kazi na kutakiwa kulipwa mafao yao ya uzeeni, hali hii husababisha wanachama kucheleweshewa malipo yao kwa makosa ambayo si ya kwao. Na wakati mwingine shirika hulazimika kuwalipa wanachama hawa kwa hasara kwa sababu waajiri wameshindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi husika.
Ili kuendana na kasi ya Mh. Rais John Pombe Magufuli na “motto” wake wa “Hapa kazi tu” shirika limeandaa mpango mkakati wa kuwapitia / kuwatembelea waajiri wote katika jiji la dsm na mikoa yote tanzania bara ambao wanadaiwa michango ya wafanyakazi wao ili kuweza kukusanya michango hiyo . Mpango  huu wa kuwatembelea waajiri hawa itaanza rasmi tarehe 2/5/2016. Maafisa wa shirika watawapitia waajiri hawa mmoja baada ya mwingine na hakuna hata mmoja atakayeachwa bila kutembelewa alimradi anadaiwa michango ya wafanayakazi.
Kumbukumbu tulizonazo, kwa mfano katika jiji la Dar es salaam  pekee mpaka mwezi machi, 2016 waajiri wapato 3,234 wanadaiwa kutowasilisha michango ya wafanyakazi wao  wenye jumla ya shs milioni 21,497.35 hali hii haiweze kuvumilika hata kidogo na ni kinyume kabisa na mwenendo kasi wa mh. Rais magufuli katika kukwaletea watanzania maendeleo endelevu na motto wake wa hapa kazi tu.
Shirika linatoa wito kwa waajiri wote kuhakikisha wanalipa michango ya NSSF ya wafanyakazi wao kwa wakati na linawataka waajiri wanaodaiwa kuhakikisha wanalipa malimbikizo yote ifikapo tarehe 30.06.2016 pia tunawaomba waajiri wote wanaodaiwa watoe ushirikiano kwa maafisa wetu pale watakapowatembelea katika  maeneo yao ya kazi ili kufikia muafaka wa pamoja wa jinsi ya kulipa madeni haya ndani ya muda uliowekwa yaani  tarehe 30.06.2016.
Itakapofika mwezi julai, 2016 shirika halitakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kuwapeleka mahakamani waajiri wote wanaodaiwa michango ya wafanyakazim, tungependa kila mwajiri atomize wajibu wake ili kuepuka usumbufu wa muda na mambo mengine lengo la nssf siku zote ni kuwa na mahusiano mazuri na waajiri na hatua za kisheria dhidi ya waajiri zinachukuliwa kama hatua za mwisho (Last resort) za kumfanya mwajiri atomize wajibu wake pale ambapo njia zingine zote zimeshindikana (zimegonga mwamba), lakini katika mazingira ya kawaida shirika halitarajii kwamba waajiri watashidnwa kutimiza wajibu wao mpaka wachukuliwe hatua za kisheria. Aidha kwa upande mwingine, serikali pamoja na vyombo vya sheria, mahakama na ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu wa serikali (DPP) wameahidi kutoa ushirikiano kwa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii – NSSF katika kutekeleza majukumu yake.
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) linapenda kutoa wito kwa waajiri wote wanaodaiwa malimbikizo ya michango ya wafanyakazi wao kulipa malimbikizo hayo kabla ya tarehe 30.06.2016.
Waajiri ni moja kati ya wadau  wakubwa wa shirika letu la NSSF kwa mujibu wa kifungu cha 11(6) na 12 (1) cha sheria ya nssf, waajiriwa wana majukumu makubwa mawili.
  1. Kuhakikisha wafanyakazi wao wanaandikishwa katika shirika la taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) mara tu wanapoajiriwa.
  1. Kuwakata michango yao asilimia 5% au 10% kutoka kwenye mshahara wa mwezi na kuwasilisha mchango huo ukiwa ni asilimia 20% ya mshahara wa mwezi, maana yake ni kwamba mwajiri baada ya kufanya makato kutoka katika mshahara wa mfanyakazi wake, anatakiwa kuongeza asilimia 10% au 15% ili ifikie asilimia 20% na kuwasilisha kwenye shirika.
Kwa mujibu wa kifungu cha 14 cha sheria ya nssf no 28 ya mwaka 1997, waajiri wote wanatakiwa wawasilishe michango ya wafanyakazi wao ndani ya siku 30 toka tarehe ya mwisho wa mwezi husika, kwa mfano mchango wa mwezi machi,2016 , unatakiwa uwe umewasilishwa kwenye shirika kabla ya tarehe 30/4/2016 kinyume na hapo ni ukiukwaji wa sheria na ni kosa la jinai.
Lakini kuna baadhi ya waajiri kwa sababu wanazozijua wenyewe, wanashindwa kutekeleza hitaji hili la kisheria kikamilifu kwa kushindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati.
Kitendo cha kutowasilisha michango ya wafanyakazi wao  kwa wakati si tu kwamba ni kosa la jinai kwa mujibu wa kifungu cha 72 (d) cha sheria ya nssf na ambayo adhabu yake ni pamoja na kifungo cha miaka 2 jela, lakini pia ucheleweshaji huu unasababisha madhara makubwa kwa wanachama na shirika kwa ujumla.
Kutowasilisha michango kwa wakati husababisha usumbufu mkubwa kwa wanachama pale wanapostaafu kazi na kutakiwa kulipwa mafao yao ya uzeeni, hali hii husababisha wanachama kucheleweshewa malipo yao kwa makosa ambayo si ya kwao. Na wakati mwingine shirika hulazimika kuwalipa wanachama hawa kwa hasara kwa sababu waajiri wameshindwa kuwasilisha michango ya wafanyakazi husika.
Ili kuendana na kasi ya mh. Rais Dk. John Pombe Magufuli na “Motto” wake wa “hapa kazi tu” shirika limeandaa mpango mkakati wa kuwapitia / kuwatembelea waajiri wote katika jiji la dsm na mikoa yote tanzania bara ambao wanadaiwa michango ya wafanyakazi wao ili kuweza kukusanya michango hiyo . Mpango  huu wa kuwatembelea waajiri hawa itaanza rasmi tarehe 2/5/2016. Maafisa wa shirika watawapitia waajiri hawa mmoja baada ya mwingine na hakuna hata mmoja atakayeachwa bila kutembelewa alimradi anadaiwa michango ya wafanayakazi.
Kumbukumbu tulizonazo, kwa mfano katika jiji la Dar es salaam pekee mpaka mwezi machi, 2016 waajiri wapato 3,234 wanadaiwa kutowasilisha michango ya wafanyakazi wao  wenye jumla ya shs. milioni 21,497.35 hali hii haiweze kuvumilika hata kidogo na ni kinyume kabisa na mwenendo kasi wa mh. Rais magufuli katika kukwaletea watanzania maendeleo endelevu na motto wake wa hapa kazi tu.
Shirika linatoa wito kwa waajiri wote kuhakikisha wanalipa michango ya NSSF ya wafanyakazi wao kwa wakati na linawataka waajiri wanaodaiwa kuhakikisha wanalipa malimbikizo yote ifikapo tarehe 30.06.2016 pia tunawaomba waajiri wote wanaodaiwa watoe ushirikiano kwa maafisa wetu pale watakapowatembelea katika  maeneo yao ya kazi ili kufikia muafaka wa pamoja wa jinsi ya kulipa madeni haya ndani ya muda uliowekwa yaani  tarehe 30.06.2016.
Itakapofika mwezi julai, 2016 shirika halitakuwa na njia nyingine ya kufanya zaidi ya kuwapeleka mahakamani waajiri wote wanaodaiwa michango ya wafanyakazim, tungependa kila mwajiri atomize wajibu wake ili kuepuka usumbufu wa muda na mambo mengine lengo la NSSF siku zote ni kuwa na mahusiano mazuri na waajiri na hatua za kisheria dhidi ya waajiri zinachukuliwa kama hatua za mwisho (Last resort) za kumfanya mwajiri atomize wajibu wake pale ambapo njia zingine zote zimeshindikana (zimegonga mwamba), lakini katika mazingira ya kawaida shirika halitarajii kwamba waajiri watashidnwa kutimiza wajibu wao mpaka wachukuliwe hatua za kisheria. Aidha kwa upande mwingine, serikali pamoja na vyombo vya sheria, mahakama na ofisi ya mwendesha mashitaka mkuu wa serikali (DPP) wameahidi kutoa ushirikiano kwa hsirika la taifa la hifadhi ya jamii – NSSF katika kutekeleza majukumu yake.

0 maoni:

Chapisha Maoni