Ijumaa, 22 Aprili 2016

SHUKURU KAWAMBWA AMWAGA MIFUKO YA SARUJI

SARUJI
Katibu wa mbunge wa jimbo la  Bagamoyo, Magreth Masenga kushoto akikabidhi mifuko ya saruji tani moja juzi kwa kwani mkuu msaidizi katika shule ya Msingi Kizuiani Nurdin Napunda wa katikati .(picha na Mwamvua Mwinyi)
…………………………………………………………………………………….
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani
MBUNGE wa jimbo la  Bagamoyo mkoani Pwani, dk Shukuru Kawambwa, ametoa tani Tatu za mifuko ya saruji katika shule  ya msingi Kizuiani, shule ya awali ya Mtoni na zahanati ya Nianjema ambapo kila sehemu imekabidhiwa tani moja moja.
Mbunge huyo ametoa mifuko hiyo kwa lengo la kutimiza ahadi yake aliyoitoa mwezi feb mwaka huu alipofanya ziara ya kutembelea shule na zahanati mbalimbali jimboni humo.
Aidha amepeleka mafuta ya dizeli Lita 200  yatakayosaidia kutumika katika gari la  shule ya sekondari fukayose.
Akikabidhi tani hizo juzi,katibu wa mbunge wa jimbo la Bagamoyo ,Magreth Masenga ,alisema walipotembelea shule ya Kizuiani walikuta walimu wa shule hiyo hawana matundu ya vyoo hali inayosababisha kujisaidia kwa mwalimu anaishi jirani na shule 
Alieleza kuwa baada ya kujionea hali hiyo isiyoridhisha mbunge huyo aliona kuna kila sababu ya kuwezesha saruji ili kusaidia kuanza kwa ujenzi kwa kushirikiana na wadau na jamii kijumla.
Magreth alisema shule ya awali ya Mtoni aliahidi kuwaunga mkono wananchi ambao walishaanza ujenzi wa darasa la  awali na lengo lao kubwa ni ianze mwaka huu.
Alisema katika zahanati ya Nianjema amepeleka tani moja kwa lengo la  kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo ambayo wakazi wa eneo hilo walianza kuijenga kwa nguvu zao ,zahanati itakayowasaidia kuwaondolea adha ya kufuata huduma ya afya mbali.
“Alipita kwenye shule hizo na zahanati ya Nianjema na kote amepeleka tani moja moja ,si kwamba atakuwa  amemaliza changamoto zao lakini itakuwa imesaidia kuendeleza pale palipobakia ” alisema Magreth kwa niaba ya dk.Kawambwa.
Magreth alisema shule ya sekondari fukayose mbunge alikuwa tatizo la   usafiri katika shule hiyo ambayo ipo  mbali na mji.
Alieleza kuwa gari lililopo shuleni hapo lilitolewa na shirika la  Goodneighbours  shirika ambalo limejenga shule hiyo lakini tatizo lilikuwa ni mafuta kwasasa .
Akizungumza changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu jimbo hapo alisema ni miundombinu kuwa chakavu kwenye baadhi ya shule,uhaba wa matundu ya vyoo na madarasa na upungufu wa walimu na madawati.
Nae mwalimu mkuu msaidizi katika shule ya msingi Kizuiani Nurdin Napunda ,alimshukuru dk Shukuru Kawambwa kwa ahadi anazotoa kwa wakati.
Napunda alisema mbunge huyo alishawahi kuwasaidiaa computer mpakato kumi na ceiling board .
Shule ya msingi Kizuiani bado inakabiliwa na upungufu wa madawa ni 421 na madarasa 19 ,upungufu uliosababishwa na ongezeko wanafunzi wa darasa la  kwanza walioandikishwa mwaka 2016.

0 maoni:

Chapisha Maoni