Ijumaa, 22 Aprili 2016

KATIBU MKUU UTUMISHI AFANYA KIKAO KAZI NA WAFANYAKAZI WA OFISI YA RAIS-UTUMISHI


U2  Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Dkt. Laurean Ndumbaro (wa pili kushoto) akifungua kikao cha Wafanyakazi wote wa ofisi ya Rais – Utumishi kilichotumika kumpata mfanyakazi bora wa ofisi kilichofanyika jana alasiri. Wengine ni Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Ofisi ya Rais-Utumishi Bw. Aloyce Msigwa(kushoto), Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora Bi. Susan Mlawi( wa pili kutoka kulia) na Katibu wa Tawi la TUGHE Utumishi Bw. Ally Litongolele (kulia).U4Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bi. Susan Mlawi akizungumza wakati wa kikao cha wafanyakazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi.
U5Katibu wa TUGHE Tawi la Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. Ally Litongolele akieleza namna ya kumpata mfanyakazi bora wa Ofisi wakati wa kikao cha wafanyakazi wote wa Ofisi ya Rais-Utumishi.
U3Kazi ya kuhesabu kura ya kumpata mfanyakazi bora wa Ofisi ya Rais-Utumishi ikiendelea.
U1Baadhi ya Watumishi wa Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma wakimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Utumishi Dkt. Laurean Ndumbaro (hayupo pichani) wakati wa kikao cha wafanyakazi wote wa Ofisi ya Rais-Utumishi kilichofanyika jana alasiri.
Picha na mpiga picha wetu

0 maoni:

Chapisha Maoni