![]() | |
| Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Iringa Bi Eunice Mmari akizungumza na wanahabari ofisini kwake leo |
![]() |
| Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Iringa Bi Eunice Mmari kushoto akizungumza na wanahabari ofisini kwake leo |
Taasisi ya
kuzuia na kupambana na Rushwa [TAKUKURU]
mkoani Iringa imewafikisha mahakamani watuhumiwa 4 kutokana na makosa
mbalimbali yanayohusu rushwa katika kesi tatu zilizofikishwa mahakanai kwa
kipindi cha Januari hadi machi mwaka huu 2016.
Akitoa
taarifa ya utendaji kazi wa Takukuru mkoa wa Iringa leo hii kwa kipindi cha
robo mwaka kuanzia juni hadi machi mwa huu kwa wandishi wa habari mkuu wa
takukuru mkoa wa Iringa Eunice Mmari alisema katika kipindi cha muhula wa miezi
mitatu takukuru ilipokea malalamiko 28 ya rushwa na 14 kati ya hayo
yamefunguliwa majalada ya uchunguzi,malalamiko 9 yakifanyiwa uchunguzi wa awali
na malalamiko 5 yameshindwa kuthibitishwa makosa ya rushwa.
Mmari
alisema Idara zinazoongoza kulalamikiwa kwa Rushwa katika mkoa wa Iringa katika ofisi za Takukuru nipamoja na Idara ya Afya na serikali za mitaa pia yapo
malalamiko kutoka Idara za ujenzi,kilimo pamoja na polisi kwa upande wa usalama
barabarani.
Alisema
watuhumiwa 4 waliofikishwa mahakani nipamoja na Lucas Daniel Mwandi ambae ni mfamasi
katika Hospital ya mkoa wa Iringa aliyeshtakiwa kwa makosa ya wizi wa mali ya
umma akiwa mtumishi wa umma kinyume na kifungu cha 270 sheria ya kanuni ya
adhabu iliyorekebishwa mwaka 2002 katika kesi Na.53/2016.
Mwigine
alifikishwa mahakani kutokana na Rushwa ni Selemani Hamza Fulano Mfamasi wilaya
ya Mufindi akishtakiwa kwa makosa ya vifungu vya 22,28 na 31 katika keasi Na.
3920016.Pamoja nao wengine wengine ni Deogratias Vangilias aliyekuwa Mwenyekiti
wa kijiji cha Mwaya Ilula na Robert Peter Kisaka aliyekuwa Mtendaji wa kijiji
cha Mwaya Ilula walioshtakiwa kwa makosa ya vifungu vya 28,31,29 NA 30 KATIKA
KESI Na.23/2016,Watuhumiowa hawa wamefikishwa mahakamani kwa makosa ya sheria
ya kuzuia na kupambana na rushwa Na.11/2007.
Taasisi
ya kuzuia na kupambana na rushwa katika mkoa wetu wa Iringa imeendelea na
utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa sheria ya kuzuia na kupambana na
rushwa kufuatia sheria namba 11 ya mwak 2007.
AlisemaUtendaji
wa kazi wa Takukuru mkoa wa Iringa kwa kipindi cha robo mwa januari hadi
machi2016 tumetoa elimu kwa umma
kwa wananchi wapatao 4957 kuhusu
vitendo vya kupambana na rushwa ikiwa nipamoja na wanafunzi 3693 kwa njia za
semina35,mikutano ya hadhara28,uimarishaji na ufunguaji wa klabu za wapinga
rushwa katika shule za msingi na sekondari46,kipindi cha radio1, na kufanya
onesho katika maeneo matatu ya manispaa ya Iringa katika wiki ya sheria
iliyoadhimishwa februari mwaka huu,pamopja na machapisho yenye ujumbe
mbalimbali wa rushwa 881 wamegawiwa kwa wananchi ili kufikisha elimu ya
rushwa.
Alisema
ofisi ya Takukuru imeweza kufanya viakao vine vya kujadili dhibiti
zilizofanyika ili kuziba mianya ya rushwa katika usimamizi wa mali za kijiji
cha Idasi,zabuni ya ununuzi wa pumpu ya kusukuma maji katika mji wa
Mafinga,ajira za vibarua katika mamlaka ya maji mji wa Mafinga na katika
taratibuy za kuchukua walimu wa kujitolea shule za msingi zilizopo Manispaa ya
Iringa na mfumo wa taratibu za matumizi ya fedha za mradi wa maji kijiji cha
Ifunda Iringa vijijini.
Aidha
alisema wameweza kufuatilia utekelezaji wa maazimio ya kudhibiti mianya ya
rushwa katika taratibu,usimamizi na matumizi ya vitendanisi katika
Hospitali,zahanati na vituop vya Afya vilivyopo manispaa ya Iringa umefanyika
katika kutekeleza majukumu yao ya kufanya uthibiti na utafiti katika maeneo
yanayohusika na vitendo vya rushwa.
Alisema
Takukuru Mkoa wa Iringa imeweka mikakati ya kuwafikia wananchi wengi zaidi ili
kutoa Elimu ya Rushwa,kwa kufanya hivyo itaweza kusaidia wananchi kuwa na
ujasili ili wajitambua kuwa na wao wanaowajibu wa kupambana na kuzuia rushwa
kwa kushirikiana na Takukuru









0 maoni:
Chapisha Maoni