...
Mkuu wa mkoa wa Iringa Bi Amina Masenza
.............................................................................................................................................................
WAKATI
baadhi ya wilaya za mkoa wa Iringa ikiwemo Iringa vijijini na
Kilolo zimekumbwa na ugonjwa wa kipindupindu kwa mwaka huu kutokana
na uchafu katika maeneo hayo ,serikali ya kata ya Mbalamaziwa wilaya
ya Mufindi mkoani hapa imeanza oparesheni ya kuwasaka wananchi
wasio kuwa na vyoo bora na kuwatoza faini ya uchafu.
Afisa
mtendaji wa kata ya Mbalamaziwa Bi Eliza Ngwaeje aliueleza mtandao
huu wa matukiodaima leo kuwa zoezi hilo ambalo limeanza kuzaa
matunda katika baadhi ya vijiji kwa wananchi ambao hawakuwa na
vyoo bora kujenga vyoo hivyo ama kuziweka vyoo vyao katika hali ya
usafi zaidi tayari limeanza katika vijiji vitano kati ya sita
vilivyopo katika kata hiyo.
Alisema
kuwa toka kamati ya afya ya kata hiyo imeanza kutekeleza zoezi
hilo wananchi wa kata hiyo wameonyesha mwitikio mkubwa wa
kutekeleza agizo hilo la usafi ambalo mara kadhaa mkuu wa mkoa wa
Iringa Bi Amina Masenza amekuwa akihimiza wananchi kuwa na vyoo bora
piakuzingatia kanuni za afya kwa kuweka mazingira safi .
Bi
Ngwaeje alivitaja vijiji ambavyo wananchi wameonyesha kutekeleza
agizo hilo la usafi kuwa ni pamoja na Kitelewasi , Idetero,
Maguvani,Ukemele na kwa kiasi kijiji cha Mbalamaziwa na kuwa kijiji
cha Nyanyembe hadi sasa bado hawajakifikia na kipo katika ratiba
ya kutembelewa kwa ajili ya ukaguzi huo wa vyoo bora na usafi.
"
Tumekuwa na changamoto kubwa ya utekelezaji wa agizo hilo kutoka
kwa baadhi ya kaya ambazo ndugu zao wapo nje ya mkoa wa Iringa
ambao wamekuwa wakiwazuia ndugu zao kutekeleza agizo hilo la
usafi na hata kufika kijijini kuitisha mkutano wa kuwazuia ndugu
zao hao kuwa na vyoo safi na bora....kweli kama viongozi tunafanya
kazi katika mazingira magumu sana katika kutekeleza agizo hili la
usafi hasa kijiji cha Mbalamaziwa ambao hawataki kutii agizo hili"
Hata
hivyo alisema kuwa kisheria kwa mujibu wa sheria za wizara ya
afya katika wilaya ya Mufindi adhabu kwa wasio na vyoo bora na
wanaopatikana na kosa la uchafu ni kati ya Tsh 50,000 hadi 200,000 ila
kutokana na waanchi hao kukubali kosa na kutekeleza agizo la usafi
kwa wakati wamekuwa wakiishia kuwatoza faini kati ya 30,000 hadi
50,0000 fedha ambazo huingizwa katika miradi ya kimaendeleo katika
kata hiyo.
Afisa
mtendaji huyo aliwataka wakazi wa Mbalamaziwa ambao wanaishi nje
ya mkoa wa Iringa kuacha kuingilia utendaji wa serikali ya kata
katika kusimamia usafi kwa wananchi wa kata hiyo kwani madhara ya
kipindupindu yakitokea ambao wataathirika ni ndugu zao ambao
wanaishi kijijini na sio wao waliopo mijini na wao kama viongozi
hawatarudi nyuma katika kusimamia suala zima la usafi kwenye kata
hiyo.







0 maoni:
Chapisha Maoni