Jumanne, 19 Aprili 2016

MVUA YASABABISHA MADHARA KAYA 156 ZAKOSA MAHALI PAKUISHI, NYUMBA 70 MBEYA.


Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya, Mch David Mwashilindi aliyevaa Suti akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa Jiji Vicent Msolla Pamoja na Naibu Meya Mch David Ngogo wakiwa wanakwenda kuwapa Pole wahanga


Mtoto akiwa amebeba vyombo mara baada ya Mvua kupungua..

Familia ikiwa inatoa Mahindi yaliyokuwa ndani ya nyumba na kuyasafisha mara baada ya Mvua Kukatika.



Mahindi yakiwa yamejaa matope..


Mwonekano wa kivuko kilichosombwa na maji katika kata ya Ilomba Kijiji cha Tonya na kusababisha  wakazi wa Kijiji cha Tonya Juu na Tonya Chini kutokupata mawasiliano


Ikawabidi kubuni Njia Mbadala



KAYA 156 katika kata ya Igawilo jijini Mbeya hazina mahali pa kuishi kutokana na nyumba zao kuzingirwa na maji kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha jijini hapa.
Mbali na kukosa mahali pa kuishi kaya hizo pia zimepoteza mali zao kadhaa yakiwemo mavazi, samani za ndani, mifugo pamoja na vyakula.
Athari hizo zimetokana na mvua zilizoanza kunyesha Aprili 15 jioni na kusababisha maeneo mengi ya Jiji la Mbeya kujaa maji na kuharibu miundombinu kadhaa yakiwemo madaraja katika kata ya Nzovwe, Ituha na Iyunga
Katika kadhia hiyo nyumba 70 zimejaa maji na tope na kusababisha wakazi wake kukosa mahali pa kuishi.
Akizungumza  Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwanyanje, Eliya Philemon, alisema athari hizo zimetokana na maji yanayotiririka kutoka maeneo ya milimani kujaa kwenye nyumba hizo kutokana na wakazi wake kujenga kwenye mikondo ya maji.
Alisema, mbali na wananchi hao kujenga kando ya mikondo ya maji pia mmiliki wa kituo cha Mafuta cha Lake Oil kilichopo katika eneo hilo ameziba mitaro inayopitisha maji kwenda kwenye mikondo ya maji hali inayochangia nyumba hizo kuzingirwa na maji.
Kutokana na hali hiyo,Mstahiki Meya wa jiji la Mbeya, David Mwashilindi, ameuagiza uongozi wa jiji kuhakikisha mmiliki wa kituo hicho anazibua mfereji huo ili kuondoa changamoto hiyo inayosababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi wa eneo.
Baaadhi ya wakazi wa eneo hilo wameulaumu ouongozi wa jiji la Mbeya kwa madai ya kushindwa kusimamia ujenzi wa makazi kwa kufuata utaratibu wa mipango miji hali iliyosababisha wananchi kujenga bila kufuata taratibu husika na hatimaye kutokea kwa kadhia hiyo.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa jiji la Mbeya, Samuel Lazaro, alisema hadi sasa bado wanaendelea kufanya tathmini kuhusu ukubwa wa kadhia hiyo ili kupata takwimu sahihi zauharibifu wa mali na athari zilizowapata wananchi hao ili kujua jukubwa na aina ya misaada wanayopaswa kuitoa kwa waathirika hao.

0 maoni:

Chapisha Maoni