Bi. Beng’i Issa Katibu Mtendaji
wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji akizungumza na waandishi wa habari
kwenye ofisi za shirika la kazi duniani ILO jijini Dar es salaam wakati
alipotangaza rasmi shindano hilo leo.
Bo Beng’i Issa Katibu Mtendaji wa
Baraza la Taifa la Uwezeshaji akizungumza na waandishi wa habari kwenye
ofisi za shirika la kazi duniani ILO jijini Dar es salaam wakati
alipotangaza shindano hio kutoka kushoto ni Nancy Lazaro Mratibu wa
Vijana ILO na katikati ni Anna marie Kiagi Mratibu wa ILO UNDAP.
Bo Beng’i Issa Katibu Mtendaji wa
Baraza la Taifa la Uwezeshaji akizungumza na waandishi wa habari kwenye
ofisi za shirika la kazi duniani ILO jijini Dar es salaam wakati
alipotangaza shindano hilo , kutoka kushoto ni Nancy Lazaro Mratibu wa
Vijana ILO na Anna marie Kiagi Mratibu wa ILO UNDAP na kutoka kushoto
ni Neema Lugangira Kaimu Mkurugenzi wa Ushiriki wa Watanzania katika
Uwekezaji na Anna Domonick Mkurugenzi wa Uwezeshaji.
…………………………………………………………………………………………………………………………..
“Ajira Yangu Business Plan
Competition” ni mpango mkakati wa kutatua changamoto za ajira kwa
Vijana, Tanzania. Mpango huu umeundwa kwaajili ya vijana kupata ujuzi wa
kuanzisha na kuendeleza biashara na kuwawezesha mitaji, ili waweze
kuanza au kuboresha biashara zao, na kutengeneza nafasi za ajira kwao
wenyewe na kwa vijana wengine pia.
Sote tunajua kuwa idadi ya vijana
katika nchi zinazoendelea kama Tanzania inaendelea kukua kwa kasi sana
na hivyo kuongezeka kwa vijana wengi wasio na ajira, hali duni ya
maisha, ukosefu wa mitaji, ukosefu wa mbinu jumuishi na kukosa fursa za
kiuchumi.
Ili kukabiliana na changamoto
zinazowakabili vijana, Shirika la Kazi Duniani (ILO) na Baraza la Taifa
la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), kwa pamoja wameunda mbinu hii
jumuishi. Ajira Yangu Business Plan Competition itahusisha vijana wenye
umri kati ya 18-35, wale wanaotaka kuanza biashara au wanaotaka kupanua
na kuboresha biashara zao.
Vijana hao watatakiwa kuja na mipango rasimu ya biashara kwaajili ya mashindano katika sekta zifuatazo;
I. Biashara ya Kilimo na kilimo usindikaji ikiwa ni pamoja na viwanda
II. Biashara inayohusu vyombo vya habari, masoko, mawasiliano, michezo, vifaa, sanaa na utamaduni, utalii na burudani.
III.Biashara inayogusa mazingira na utunzaji wa mazingira ikiwa ni pamoja na biashara ya kijamii.
IV. Biashara inayohusu habari na
mawasiliano, teknolojia ikiwa ni pamoja na usindikaji biashara Taratibu
za Uombaji. Taratibu za uombaji itahusisha awamu tatu.
Awamu ya kwanza itahusisha kujaza
fomu ya maombi inayopatikana ndani ya tovuti ya Shirika la Kazi Duniani
(ILO) na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi(NEEC)
. Maombi yataanza kupokelewa
kuanzia Aprili 18 mpaka Mei 9, 2016. Awamu ya pili itahusisha mafunzo ya
biashara. Vijana ishirini na tano waliochaguliwa kutoka awamu ya 1
watapitia mafunzo ya kina kwa siku moja juu ya mipango ya biashara.
Mafunzo haya yatakuwa kwaajili ya
vijana wote ishirini na tano waliochaguliwa ili kunoa ujuzi wao katika
mipango ya biashara ambayo itasababisha kuendeleza mipango yao ya
biashara.
Matokeo muhimu ya mafunzo hayo,
itakuwa ni kwa kila mshiriki kuandaa, kuongeza na kuboresha mpango
kamili wa biashara. Awamu ya tatu ya , Ajira Yangu Business Plan
Competition itahitimishwa kwa kuwakutanisha washiriki wote ishirini na
tano. Washiriki ishirini na tano waliochaguliwa watawasilisha mawazo
bunifu ya biashara zao mbele ya washauri, majaji, wawekezaji walioalikwa
pamoja na wananchi wengine.
Kila mshiriki atapata fursa ya
kujieleza kuhusu safari yake ya ujasiriamali na mafanikio yake ya
baadaye. Na mchango wa biashara yake katika kujenga ajira kwa wengine.
Baada ya hapo, majaji watachagua mawazo ya biashara iliyo bunifu na
yenye uvumbuzi kuliko wote.
Washindi wa Ajira Yangu Business
Competition watatangazwa baada ya majaji kupendekeza marina yaliyokizi
vigezo vilivyopo.Washiriki wote watapokea msaada wa kiufundi na
kitalaamu ili kukuza biashara zao kwa mwaka mmoja. Miongoni mwa
washiriki ishirini na tano, washiriki sita wenye mawazo ya ubunifu
watachaguliwa na kila mmoja atapokea tuzo kwa njia ya mtaji ili
kuwawezesha kuanzisha au kuendeleza biashara zao, na kujenga ajira zao
wenyewe na kwa wengine.
Baada ya hapo, majaji watachagua
mawazo ya biashara iliyo bunifu na yenye uvumbuzi kuliko wote. Washindi
wa Ajira Yangu Business Competition watatangazwa baada ya majaji
kupendekeza marina yaliyokizi vigezo vilivyopo.Washiriki wote watapokea
msaada wa kiufundi na kitalaamu ili kukuza biashara zao kwa mwaka mmoja.
Miongoni mwa washiriki ishirini na tano, washiriki sita wenye mawazo ya
ubunifu watachaguliwa na kila mmoja atapokea tuzo kwa njia ya mtaji ili
kuwawezesha kuanzisha au kuendeleza biashara zao, na kujenga ajira zao
wenyewe na kwa kwa wengine. Lengo la Ajira Yangu Business Plan
Competition ni kuongeza idadi ya vijana wanawake kwa wanaume katika
biashara na kuzalisha kazi na ajira.
0 maoni:
Chapisha Maoni