Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli
wakiwa na wenyeji wao Rais Paul Kagame na Mama Janeth Kagame wakiwasili
katika viwanja vya Kumbukumbu ya Mauaji ya Kimbali mjijini Kigali,
Rwanda, leo katika maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka
22 ya mauaji hayo yaliyotokea mwaka 1994 ambapo watu takribani milioni
1,000,000 waliuawa.
22 ya mauaji hayo yaliyotokea mwaka 1994 ambapo watu takribani milioni
1,000,000 waliuawa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli
wakishuhudia wenyeji wao Rais Paul Kagame na Mama Janeth Kagame pamoja
na binti yao wakiweka shada la maua katika viwanja vya Kumbukumbu ya
Mauaji ya Kimbali mjijini Kigali, Rwanda, leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli
wakiweka shada la maua wakishuhudiwa na wenyeji wao Rais Paul Kagame na
Mama Janeth Kagame wakiweka shada la maua katika viwanja vya Kumbukumbu
ya Mauaji ya Kimbali mjijini Kigali, Rwanda, leo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt John Pombe Joseph Magufuli na Rais Paul Kagame kwa pamoja
wakiwasha “Urumuri Rutazima” (Mwenge/mwali wa Matumaini) katika
maadhimisho Kumbukumbu ya miaka 22 ya Mauaji ya Kimbali mjijini Kigali,
Rwanda, leo
Maafisa utamaduni wametakiwa kushirikiana na wasanii kuboresha sanaa ili itumike kutangaza maeneo ya utalii wa utamaduni yaliyopo nchini
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza na wadau wa kada
anazozisimamia alipofanya ziara jana Mkoani Geita na kukutana na wadau
hao pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa wa Geita.
Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Manzie Magochie na kulia ni
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Herman Matemu
Baadhi ya wadau wa sekta ya
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo pamoja na watendaji wa serikali Mkoa
wa Geita wakifurahia hotoba iliyotolewa na Waziri wa Habari,Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipofanya ziara jana Mkoani Geita
kukutana na wadau hao pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari
wa mkoa wa Geita.
: Meneja wa Mamlaka ya
Mawasiliano (TCRA) Kanda ya ziwa Eng. Lawi Odiero(aliyesimama) akijibu
hoja wakati wa ziara ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Mhe. Nape Nnauye (kulia) kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia jana
Mkoani Geita. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Manzie Magochie
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (watatu kushoto) akiwasili katika
kiwanja cha michezo cha jiji alipofanya ziara jana Mkoani Geita kukutana
na wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kuangalia miundombinu ya
viwanjwa vya michezo mkoani humo. Watatu kulia ni Mkuu wa Wilaya ya
Geita Mhe. Manzie Magochie
Waziri wa Habari, Utamaduni,
Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (katikati) katika picha ya pamoja na
waandishi wa habari wa Mkoa wa Geita baada ya kukutana nao jana mkoani
hapo na kujadili fursa pamoja na changamoto mbalimbali zinazokabili
sekta anazozisimamia. Kulia kwa Waziri ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe.
Manzie Magochiena kulia ni Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda
ya ziwa Eng. Lawi Odiero.
Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo, Geita
………………………………………………………………………………………………
Na: Genofeva Matemu – Geita, Maelezo
Maafisa utamaduni nchini
wametakiwa kushirikiana na wadau pamoja na kuandaa vikao vya mara kwa
mara na wadau wa utamaduni wakiwemo wasanii ili kuweza kujenga ukaribu
na kutoa elimu ya sanaa itakayosaidia kuboresha kazi za sanaa hivyo
kutumia sanaa kutangaza maeneo ya utalii wa utamaduni yaliyopo nchini.
Hayo yamesemwa na Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipokutana na
wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa
habari jana Mkoani Geita.
Mhe. Nnauye amesema kuwa kama
maafisa utamaduni watakua karibu na wadau wa sanaa na utamaduni ujuzi wa
tasnia ya sanaa na utamaduni utaongezeka kwa kujifunza kutoka kwa mtu
mmoja kwenda kwa mwingine hivyo kukuza vipaji vya wasanii
vitakavyotumika kutangaza maeneo ya utalii wa utamaduni na kuvutia
watalii pamoja na wawekezaji.
Aidha Mhe. Nnauye ameitaka jamii
kuheshimu kazi za sanaa na kuwathamini wasanii kwani serikali inampango
wa kurasimisha kazi za sanaa hivyo kuifanya sanaa kuwa shughuli rasmi
ya kiuchumi itakayowawezesha wawekezaji kuwekeza katika sanaa na
kumfanya msanii apate kipato kizuri lakini pia kuiwezesha serikali
kupata kipato kupitia tasnia ya sanaa na utamaduni.
Naye Mwenyekiti wa chama cha
Waigizaji Mkoa wa Geita Bibi. Rosemery Michael amemuomba Mhe. Waziri
kuhakikisha kuwa wasanii wanapata usajili na kuwa na uhalali wa kufanya
kazi zao kwa kuhakikisha kuwa wasanii wanafuata sheria na taratibu
zitakazowapa muongozo wa kufanya shughuli zao kwa ufanisi na weledi
hivyo kuwaongezea kipato.
Bibi. Michael amesema kuwa tasnia
ya sanaa inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo kutokuwa na chuo cha
sanaa mikoani, wasanii kutokua na elimu ya sanaa itakayowajengea uwezo
wa kujikwamua kiuchumi, wasanii kufanya kazi kiholela, pamoja na uhaba
wa uwekezaji katika tasnia ya sanaa.
Aidha Katibu wa Chama cha
waigizaji Mkoa wa Geita Bw. Kangeta Ismaili ameomba mfuko wa maendeleo
ya vijana kutambua vikundi vya wasanii na kuvifikia vikundi hivyo kwa
kuwapa mikopo ambayo itawawezesha kuboresha kazi za sanaa na kuwainua
wasanii kiuchumi.






0 maoni:
Chapisha Maoni