Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akisaini kitabu
cha wageni alipowasili katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.
Anthony John Mtaka (kushoto) jana wakati wa ziara yake mkoani hapo
kukutana na wadau wa sekta anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi
kwa maafisa habari wa mkoa huo.
Kaimu
katibu msaidizi CCM Mkoa wa Simiyu Bw. Gelison Nyamwihula akitoa
taarifa ya chama mkoani simiyu kwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo Mhe. Nape Nnauye (katikati) alipotembelea ofisi za CCM jana
mkoani humo. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony John Mtaka
Katibu
Tawala Mkoa wa Simiyu Bibi. Mwamvua Jilumbi (aliyesimama) akitoa
taarifa ya Mkoa wa Simiyu upande wa sekta za Habari, Utamaduni, Sanaa na
Michezo kwa waziri mwenye dhamana na sekta hizo Mhe. Nape Nnauye
(kushoto) alipofanya ziara jana mkoani hapo kujua hali ya sekta hizo
pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa huo.
Wapilikushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony John Mtaka
Meneja
wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda ya ziwa Eng. Lawi Odiero
(aliyesimama) akijibu hoja wakati wa ziara ya Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye kukutana na wadau wa sekta
anazozisimamia jana Mkoani Simiyu.
Waziri
wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akikagua iPad
kabla ya kumkabidhi afisa habari wa Mkoa wa Simiyu Bibi. Stella Kalinga
(kulia) wakati wa ziara yake mkoani humo kukutana na wadau wa sekta
anazozisimamia jana Mkoani Simiyu.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye
(kushoto) akizungumza na waandishi wa Mkoa wa Simiyu baada ya kufanya
ziara yake jana mkoani humo kwa kukutana na wadau wa sekta
anazozisimamia pamoja na kutoa vitendea kazi kwa maafisa habari wa mkoa
huo.
Picha na: Genofeva Matemu – Maelezo, Simiyu
………………………………………………………………………………………….
Na: Genofeva Matemu – Maelezo, Simiyu
Vyombo
vya habari nchini vimetakiwa kuandaa vipindi vya kuelimisha na
kupunguza burudani kwa kuongeza idadi ya vipindi vya kujenga uzalendo,
amani, mshikamano pamoja na umoja wa kitaifa
Rai
hiyo imetolewa na Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda ya Ziwa
Eng. Lawi Odieri wakati wa ziara ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa
na Michezo Mhe. Nape Nnauye alipokutana na wadau wa sekta anazozisimamia
jana Mkoani Simiyu.
“Mamlaka
ya mawasiliano inafuatilia kwa karibu maudhui ya vyombo vya habari ili
kuepusha maudhui potofu na hatarishi yatakayoweza kuondoa mshikamano na
uzalendo tulio nao” alisema Eng. Odieri
Aidha
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ameiagiza Mamlaka ya
Mawasiliano (TCRA) kutoa uwepo wa masafa ya kuanzishia vituo vya
utangazaji katika Mkoa wa Simiyu pamoja na mikoa mingine ya jirani ili
kuweza kuongeza idadi ya vituo vya utangazaji ambapo kwa mkoa wa Simiyu
hadi sasa kuna kituo kimoja tu cha utangazaji.
Mhe.
Nauye amesema kuwa uwepo wa vituo vya kutosha vya utangazaji katika mkoa
wa Simiyu vitasaidia kutangaza vivutio vya utalii wa kiutamaduni
vilivyopo mkoani Simiyu pamoja na kuinua wasanii wa mkoa huo kwa
kuwapatia nafasi ya kurusha nyimbo zao katika vituo hivo.
Mpaka
sasa idadi ya vituo vya redio nchini zenye leseni imeongezeka na
kufikia vituo 123, wakati idadi ya vituo vya televisheni zenye leseni
katika mfumo wa dijitali nchini umefikia 26 huku kanda ya ziwa ikiwa na
jumla ya vituo vya redio 23 na kituo kimoja cha televisheni.
0 maoni:
Chapisha Maoni