Jumanne, 19 Aprili 2016

Halmashauri yatenga bajeti ya milioni 162 kuisaidia shule ya walemavu


03 mnazi mmoja Lindi
Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Halmashauri ya Wilaya ya Lindi iliyopo Mkoa wa Lindi imetenga jumla ya shilingi milioni 162 katika mwaka wa fedha 2016/17 kwa ajili ya kuisaidia shule ya Msingi Nyangao.
Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Olliver Vavunge alipokuwa akikanusha kuhusu madai ya wazazi kutaka shule hiyo ifungwe kwa sababu ya ukosefu wa huduma muhimu.
“Kwa kuwa shule hiyo tayari ina mabweni pamoja na bwalo la chakula, katika bajeti iliyotengwa na Halmashauri kwa mwaka huu wa fedha jumla ya shilingi milioni 100  zitatumika katika ujenzi wa uzio wa shule pamoja na marekebisho madogo madogo ya shule hiyo na shilingi milioni 62 zitatumika kwa ajili ya chakula”alisema Bi. Olliver
Aidha, Bi. Olliver amekanusha kupewa bajeti ya  shilingi laki tisa kwa ajili ya matumizi ya shule hiyo kwa mwezi kama ilivyoripotiwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari na kusema kuwa Serikali inatoa jumla ya shilingi milioni 1.6 kwa kila mwezi.
Ameongeza kukanusha kuwa si kweli kuwa wanafunzi wanakula mlo mmoja kwa siku bali wanapata milo yote mitatu kama ilivyo kawaida.
 
Shule ya Msingi Nyangao ni shule ya watoto wenye mahitaji maalumu (walemavu) ambayo hadi sasa ina jumla ya wanafunzi 42 na inahudumiwa na Serikali kwa mahitaji yote.

0 maoni:

Chapisha Maoni