Na Jacquiline Mrisho – MAELEZO
Halmashauri ya Wilaya ya Lindi
iliyopo Mkoa wa Lindi imetenga jumla ya shilingi milioni 162 katika
mwaka wa fedha 2016/17 kwa ajili ya kuisaidia shule ya Msingi Nyangao.
Hayo yamesemwa leo na
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi. Olliver Vavunge alipokuwa
akikanusha kuhusu madai ya wazazi kutaka shule hiyo ifungwe kwa sababu
ya ukosefu wa huduma muhimu.
“Kwa kuwa shule hiyo tayari ina
mabweni pamoja na bwalo la chakula, katika bajeti iliyotengwa na
Halmashauri kwa mwaka huu wa fedha jumla ya shilingi milioni 100
zitatumika katika ujenzi wa uzio wa shule pamoja na marekebisho madogo
madogo ya shule hiyo na shilingi milioni 62 zitatumika kwa ajili ya
chakula”alisema Bi. Olliver
Aidha, Bi. Olliver amekanusha
kupewa bajeti ya shilingi laki tisa kwa ajili ya matumizi ya shule hiyo
kwa mwezi kama ilivyoripotiwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari na
kusema kuwa Serikali inatoa jumla ya shilingi milioni 1.6 kwa kila
mwezi.
Ameongeza kukanusha kuwa si kweli kuwa wanafunzi wanakula mlo mmoja kwa siku bali wanapata milo yote mitatu kama ilivyo kawaida.
Shule ya Msingi
Nyangao ni shule ya watoto wenye mahitaji maalumu (walemavu) ambayo hadi
sasa ina jumla ya wanafunzi 42 na inahudumiwa na Serikali kwa mahitaji
yote.
0 maoni:
Chapisha Maoni