Jumanne, 19 Aprili 2016

Uchukuzi SC netiboli kuivaa CDA Dodoma leo


UC2Kocha wa soka Elutery Muholeli (wanne kulia) mwenye jezi za manjano akitoa maelekezo kwa wachezaji.
UC3
Mazoezi mpira wa Netball  yakiendelea 
UC4Matalena Mhagama (mwenye fulana nyeupe kulia) akisubiri mpira.
…………………………………………………………………………………………………………
Mwandishi Wetu
TIMU ya netiboli ya Uchukuzi SC iliyopo chini ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kesho itarusha karata yake ya kwanza kwa kuumana na wenyeji CDA Dodoma katika mchezo wa netiboli, utakaofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri.
Uchukuzi SC iliyoundwa na wachezaji mahiri imekuwa katika mazoezi ya muda mrefu, huku ikipata mechi kadhaa za kirafiki dhidi ya timu maarufu ya Cargo na Uhamiaji zote za jijini Dar es Salaam.
Kocha Mkuu wa timu hiyo, ambaye pia ni mchezaji wa zamani wa Bandari na timu ya Taifa, Judith Ilunda alisema wamekuja kushindana na sio kuwa wasindikizaji, ambapo wanatarajia ushindi mnono dhidi ya wapinzani wao.
Hatahivyo, Ilunda alisema CDA sio timu ya kubeza kwani inaundwa na wachezaji wazoefu, wenye kujua mbinu mbalimbali za uchezaji, hivyo atahakikisha wachezaji wake watacheza kwa tahadhari, ili kuibuka na ushindi.
“Tumekuja kushindana huku na kamwe hatutakubali kuwa wasindikizaji, hivyo nitahakikisha wachezaji wangu wanajituma kila idara ili tushinde kwani hii timu tunayocheza nayo inawachezaji wakongwe na wenye uzoefu,” alisema Ilunda.
Aliwataja wachezaji wanaounda kikosi mahiri na nafasi zao uwanjani kuwa ni Matalena Mhagama (GA), Subira Jumanne (WD), Mwadawa Hamis (GD), Sharifa Mustafa (GK), Mary Kajigiri (WA) na Mayasa Hamidu .
Wachezaji wengine ni Grace Mwasote (GS), Neema Makassy (WD), Johari William (GK), Salama Mbuguni (WA), Mwanaisha Athuman (WD) na Tatu Kitula (GS).
Timu hiyo mwaja jana katika mashindano ya Mei Mosi iliyofanyika Mwanza ilishika nafasi ya pili, baada ya kukutana na Utumishi katika fainali.
Michezo hii ya Mei Mosi, ambayo ilianza jana (Jumanne) inazinduliwa rasmi leo (Jumatano) na mgeni rasmi mkuu wa mkoa, Jordan Rugimbana.

0 maoni:

Chapisha Maoni