JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
Ndugu wanahabari,
Kila
wiki serikali kupitia Wizara yangu imekuwa ikitoa taarifa ya mwenendo wa
mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu na hatua zinazochukuliwa kudhibiti
ugonjwa huu. Aidha pia kila mwisho wa mwezi, majumusiho hufanyika na
kutolewa taarifa. Hadi kufikia tarehe 4 April 2016, jumla ya wagonjwa
20,294 wametolewa taarifa, na kati ya hao 320 wamepoteza maisha
Kwa
kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka, mwenendo wa Kipindupindu unaashiria
kuwa idadi ya wagonjwa inaongezeka nchini. Mwezi Januari kulikuwa na
wagonjwa 2,272, na mwezi Machi kulikuwa na wagonjwa 2,956. Hili ni
ongezeko la asilimia 30.1%. Hata hivyo, baadhi ya mikoa imeonyesha
uendelevu wa kupungua kwa idadi ya wagojwa wa Kipindupindu kwa robo ya
kwanza. Mikoa hiyo ni pamoja na Simiyu, Rukwa na Mbeya. Takwimu hizi za
nchi nzima zinaashiria kuwa juhudi za kupambana na ugonjwa wa
Kipindupindu zinahitaji
kutekelezwa
na kusimamiwa kikamilifu na mikoa na wilaya zote nchini baada ya Wizara
yangu kutoa maelekezo na miongozo stahili. Vile vile, napenda
kusisitiza kwamba hata Mikoa ambayo haina wagonjwa ni lazima wachukue
hatua za tahadhari kuzuia maambukizi mapya, na ile mikoa ambayo ina
wagonjwa iendelee kusimamia kikamilifu udhibiti wa mlipuko.
Katika
mwezi Machi, jumla ya wagonjwa wapya walioripotiwa nchi nzima walikuwa
2,956, na vifo vilikuwa 53. Takwimu za mwezi Machi (tarehe 5 Machi hadi 3
Aprili) zinaonyesha idadi ya wagonjwa imeongezeka kwa asililmia 59.5%
ikilinganishwa na idadi ya wagonjwa wa mwezi Februari (1,853). Mikoa ya
Tanga, Pwani na Mtwara haikuwa imeriporti wagonjwa mwezi wa Februari
lakini mwezi huu wa Machi imepata wagonjwa wapya. Aidha katika kipindi
hiki cha mwezi mmoja kumekuwa na ongezeko kubwa la wagonjwa wapya kwenye
mikoa ya Geita, Kilimanjaro, Manyara, Morogoro, na Dodoma. Idadi ya
wagonjwa kutoka mikoa ya Simiyu, Mbeya na Iringa imepungua kati ya
Februari na Machi 2016.
Kwa
upande wa takwimu za kila wiki (weekly report), idadi ya wagonjwa wa
Kipindupindu walioripotiwa kwa wiki ya kati ya tarehe 28 Machi hadi 3
Aprili 2016 imepungua kwa asilimia 37.2 ikilinganishwa na idadi ya
wagonjwa walioripotiwa kati ya tarehe 21 hadi 27 Machi 2016. Kwa wiki
hii ya tarehe 28 Machi hadi 3 Aprili 2016 kulikuwa na jumla ya wagonjwa
wapya 430 na vifo saba (7). Idadi ya vifo kwa wiki hii imeongezeka
kutoka vifo vinne vilivyoripotiwa katika wiki iliyopita. Kwa wiki hii
mikoa iliyopata wagonjwa wengi zaidi ni Kilimanjaro (128), Mara (102),
Morogoro (67), Geita (46), Mwanza (40) na Dar es Salaam (31).
Halmashauri kumi zilizoongoza kwa idadi ya wagonjwa wapya wiki hii ni
Same (74), Tarime Vijijini (52), Moshi Vijijini (44), Mvomero (27),
Rorya2






0 maoni:
Chapisha Maoni