Jumanne, 5 Aprili 2016

SHUHUDIA UPONYAJI WA MAOMBEZI YA ASKOFU E.A. KALINGA WA KANISA LA SINAI KIMARA TEMBONI DAR ES SALAAM

1Askofu E. A.Kalinga pamoja na mkewe Mch Christina A.Kalinga kwa pamoja wakishuhudia muujiza wa mtoto aliye zaliwa Baada ya  maombezi,  katika picha mtoto Baraka Peter Lugega akiwa  amebebwa na Baba yake Bw. Peter Legega ,pamoja na Mama yake Eva Katikati  Wakiwa Kanisani.Baada ya Bw. Peter Lugega kuponywa pepo la ulevi uliopindukia na mke wake aliyepoteza Mimba sita na alikuwa hajawahi kunyonyesha mtoto  lakini baada ya kuombewa na kuponywa  anashangaa sasa ananyonyesha mtoto aliyejifungua baada ya maombezi hayo.
Maeneo  tulipo : Morogoro Road  Kimara Temboni  Wilaya   ya Kinondoni  kabla   ya  Mbezi  mwisho, Saranga,hatua chache utaona kibao  chetu  barabara ni-Kushoto   rangi ya blue  bahari.
6:  Huduma zetu Kanisani:- Jumapili asubuhi saa 2:00 -4:30 watu wote  kujifunza  neno  la Mungu ,Sunday School.
;saa 4:30-5:30 kusifu na kuabudu na mambo mengine (ibada ya kawaida) 5:30-6:30 maombi ya udhihilisho wa nguvu ya Mungu katikati ya kusanyiko (ibada) -kujazwa Roho Mtakatifu (watu wote) -kunena kwa lugha  mpya(watu wote) -kuponywa  magonjwa  mbalimbali (watu wote)  -kufunguliwa  vifungo vya uovu vya asili,na  laana mbalimbali za  watu (watu wote)  2: Jumatano: Hii  ni siku  ya  watumishi  kuwepo Kanisani  kuanzia   Saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni kwaajili ya :-   -Ushauri  wa mtu mmojammoja (Canseling)  -maombi ya kufungua  vifungo vya uovu kwa watu mbalimbali na laana    Mbalimbali -kuombea wagonjwa na kuponywa  -kusikia shuhuda  mbalimbali  kwa watu Mungu alivyo watendea.  3:  Ijumaa siku hii  ya ibada  inaanza  saa 10:00- 12:00 jioni  tunasifu na Kuabudu ,na kusikia  neno  la Mungu ,na Maombi.
Napenda kueleza kwa wale  wenye  mapenzi mema kwa huduma yetu .Sisi tumepata bure  Tunatoa bure watu hawa tunao wahudumia ,au tulio wahudumia si matajiri ni watu wa kawaida kama umeguswa na huduma yetu unaweza kuchangia huduma hii ili iwafikie watu wengi zaidi.
Namba zetu za simu unaweza  kutuma chochote,au kwa mazungumzo nasi   Voda: 0767919056  – Tigo:0712964258  Airtel :0692567672.
2
Askofu  E.A.Kalinga  aliye simama upande wa kulia katika picha, wakiwa  katika picha ya pamoja  na Wachungaji.  Baada ya kuwabariki   katika Kanisa la Sinai  Tanzania Mkoa wa Rukwa, Sherehe hiyo ilihudhuriwa  na viongozi wa Serikali pia ,aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga mjini  Meja Mstaafu Bahati Matala  ambaye  wameshikana mikono kwa furaha pamoja na viongozi wa Kata ya Malangali Wilaya ya Sumbawanga Mjini  wakiwa pamojana  baadhi ya niongozi wa Kanisa.
3
Baadhi ya waumini ndani ya kanisa wakijifunza neno la Mungu  kipindi cha Sunday School ambacho kimekuwa  chenye  baraka sana  ya watu kulijua neno la Mungu kwa kina .
4
Askofu E.A Kalinga pamoja na mke wake Mchungaji Christina Kalinga  waliokaa  viti vya mbele  pamoja na  baadhi ya waumini  wakiwa katika  hafla ya pamoja wakisherehekea baada ya ubatizo katika Kanisa hilo. Hili ni jambo linalo leta furaha katika utumishi, baada ya kuwafundisha watu neno la Mungu na kuelewa  na kukubali kubatizwa.Math 28:19-20;Mark 16:15-16.
5
Waumini waliobatizwa  wakiwa katika picha ya pamoja  na Askofu Kalinga  na mke wake Mchungaji Christina Kalinga ,  wakisherehekea  baada ya  ubatizo wao uliofanyika kwa  Mchungaji Sekela Mushi wa kanisa la Penuel lililoko Suka  -Kimara Dar es Salaam.
6
Askofu E.A Kalinga akimbatiza Mmoja wa waumini waliokata shauri na kubatizwa na askofu huyo wa kanisa la Sinai Dar es salaam kwa ubatizo wa maji mengi (kuzamisha).   
7
Askofu .E.A.Kalinga  kulia akiwa  katika picha ya  pamoja na wanachuo wenzake wakati wa  walipohitimu  shahada  ya Diploma, katika  chuo cha Bibilia  cha The Oasis  Healing  Bible  College,  kilichopo  nyuma  ya  jengo la  ubungo Plaza, karibu na stendi  ya  mabasi yaendayo mikoani  hapa Dar es Salaam.

0 maoni:

Chapisha Maoni