Jumatano, 12 Oktoba 2016

TANZANIA NA MAREKANI KUDHIBITI BIASHARA HARAMU YA BINADAMU

Posted by Esta Malibiche on Oct12.2016 in NEWS

001
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya, akizungumza na Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu, Carl Fox, baada ya kumtembelea naibu katibu mkuu ofisini kwake kwa lengo la kujadili ushirikiano wa Tanzania na Marekani katika kudhibiti biashara hiyo.Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
002
Naibu Mkurugenzi wa Kitengo cha kupambana na Biashara Haramu ya Usafirishaji wa Binadamu, Carl Fox  akizungumza na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Simba Yahya, baada ya kumtembelea Naibu Katibu Mkuu ofisini kwake kwa lengo la kujadili ushirikiano wa Tanzania na Marekani katika kudhibiti biashara hiyo. Wa kwanza kushoto ni Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu kutoka wizarani , Seperatus Fella na wengine ni wajumbe walioongozana na Naibu Mkurugenzi kutoka ubalozi wa Marekani. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
003
Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi , Seperatus Fella akizungumza na  Naibu Mkurugenzi kitengo cha kupambana na kuzuia usafirishaji binadamu, juu ya  hali ya biashara haramu ya usafirishaji binadamu  nchini na namna ambavyo wanashirikiana na taasisi mbalimbali  kuzuia na kutokomeza  biashara hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
004
Katibu wa Kamati ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu kutoka  Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Seperatus Fella (kulia), akimsikiliza Naibu Mkurugenzi kitengo cha kupambana na kuzuia usafirishaji binadamu nchini Marekani,  Carl  Fox, aliyeambatana na ujumbe  kutoka ubalozi wa Marekani nchini kwa lengo la kujadili ushirikiano wa Tanzania na Marekani katika kudhibiti biashara hiyo. Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

0 maoni:

Chapisha Maoni