Jumanne, 18 Oktoba 2016

WANANCHI WILAYANI KILOLO NA IRINGA DC WANUFAIKA NA ELIMU YA UMILKI ARDHI KUTOKA SHIRIKA LA PELUM TANZANIA

Posted by Esta Malibiche on Oct 19.2016 in NEWS
Meneja wa  shirika la Pelum Tanzania  Rehema Fidelis akitoa  maelezo kuhusu shirika  na mradi kwa wananchi  ][hawapo pichani]wa wilaya ya Kilolo Mkoani Iringa wakati wa mdahalo  ulioandaliwa na shirika la PELUM uliofanyika wilayani Kilolo ukiwahusisha wananchi wa Wilaya ya Kilolo na Iringa Dc
Alisema lengo la mradi wa Pelum ni kuhakikisha wananchi wanakuwa na uelewa kuhusu ardhi.
Alisema Shughuli kuu ya Pelum Tanzania ni kuhakikisha  kilimo kinaendelezwa kwa kutumia mikakati ya kujenga na kuimarisha uwezo wa wa mashirika  ya uanachama hasa katika masuala yanayohusu matumizi endelevu ya ardhi.

 


 Washiriki wa mdahalo wakiendelea kusikiliza mada mbalimbali zinazowasilishwa


 Mdahalo ukiendelea



 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilolo Yusuph Msawangaakifungua Mdahalo huo, aliwataka washiriki  kutumia fursa hiyo kutoa changamoto zilizopo katika sekta ya ardhi kama njia ya kuzitafutia ufumbuzi



 Akiwasilisha mada katika mdahalo huo Afisa mradi wa Pelum Tanzania Angolile Rayson alisema utafiti uliofanywa na shirika hilo mwaka 2014 katika wilaya ya Kilolo ulibaini kuwa migogoro ya ardhi ya kwa wananchi wanaogombea mipaka katika maeneo ya vijijini ni asilimia 61 ya migogoro yote.





Washiriki wa mdahalo wakiendelea na majadiliano,ambapo Joseph Peter alisema kuwa ili Migogolo ya ardhi iweze kumalizika  ardhi inayomilikiwa na wananchi  inatakiwa kupimwa na kupewa hati miliki za kimira kwa mtu mmoja mmoja.w

 Katika kuchangia kwake Mjadala Rashid Abdalah alisema  sheria na taratibu za umiliki ardhi zinatakiwa kufuatwa pamoja na usimamizi wa utekelezaji wa wajibu wa Ardhi.Pia alisema kuondokana na migogoro ya ardhi miongoni mwa watumiaji wa ardhi vijijini Elimu ya umiliki Ardhi inatakiwa kutolewa kwa wananchi.






Wananchiwakiendelea  kuchangia mawazo katika ,kutokana na mada iliyosema nini kifanyike kuhakikisha Migogoro ya ardhi inaisha
 Mada mbalimbali zonazohudu haki ya umiliki ardhi zikiendelea kutolewa na muwezeshaji   ambae pia ni Mratibu wa shirika la Pelum
  Kwa upande wake Bahati Mkove aliiomba serikali kutenga maeneo baina ya wakulima na wafugaji  waliopo vijijin.Pia alisema kuwa  ni vema Halmashauri na viongozi wa kijiji wakashirikiana kwa pamoja wakati wa kupima ardhi na kumilikisha maeneo ili kuepusha na Migogoro kutokea





0 maoni:

Chapisha Maoni