Jumamosi, 8 Oktoba 2016

DC SOPHIA MJEMA AKUTANA NA WAJUMBE WA BARAZA LA ARDHI ILALA


Posted  by Esta Malibiche on Oct8.2016 in NEWS

 

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sophia Mjema amekutana na wajumbe wa baraza la ardhi la wilaya hiyo na kupanga mikakati ya kutatua migogoro katika kata mbalimbali. 


Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake jana Mjema alisema kuwa kuanzia sasa ataanza kuzunguka na wajumbe hao wa baraza katika kata mbalimbali ili waweze kujionea kwa macho tatizo la migogoro ya ardhi linalo wakabili. 
“Hiki ni kikao cha kawaida tu chenye lengo la kupanga mipango mbalimbali ya kutatua changamoto zinazo wakabili wakazi wa Ilala haswa Migogoro ya ardhi” anasema Dc Sophia Mjema 
Alisema lengo la ziara ni pamoja na kujenga mshikamano wa kikazi baina ya wananchi na Watendaji wa Serikali katika kutatua kero zao.
Ilala Dar es salaam,Tanzania.

0 maoni:

Chapisha Maoni