Jumamosi, 29 Oktoba 2016

HANS POPE AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO VYENYE THAMANI YA MILL.2,900000 KWA KIKOSI CHA JESHI LA ZIMAMOTO IRINGA

Posted by Esta Malibiche on Oct 29.2016 in MICHEZO
Akimkabidhi,Siza Hans Pope akimkabidhi  vifaa vya Michezo Mratibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Iringa,Kennedy komba kwa niaba ya
Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa timu ya Simba Hans Pope.
 Siza Hans Pope akimkabidhi  vifaa vya Michezo Mratibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Iringa,Kennedy komba kwa niaba ya Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa timu ya Simba Hans Pope
 
 Jezi seti nne zilizotolewa na mdau wa Michezo Nchini Hans Pope kwa Jeshi la Zima moto



Siza Hans Pope akizungumza na kikosi cha jeshi la Zimamoto mara baada ya kukabidhi vifaa vya Michezo
Mratibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Iringa,Kennedy komba mara baada ya kupokea Msaada wa vifaa vya Michezo kutoka kwa Madu wa Michezo,Hans Pope iliyokabidhiwa na Siza Hans Pope
Hilaly Kobelo ni Mkaguzi Msaidizi wa Zimamoto mkoa wa Iringa,ambae pia ni nahodha wa kikosi  cha Timu hiyo alisema kuwa, kikosi hicho kilikuwa kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wavifaa vya michezo hivyo msaada huo utawasaidia katika kujiandaa na michezo mbalimbali



 



 
 



 





 

 





Picha zote na Esta Malibiche[KALI YA HABARI BLOG]



Na Esta Malibiche
Iringa
Mwenyekiti wa kamati ya Usajili wa timu ya Simba Hans Pope amekabidhi vifaa vya Michezo vyenye thamani ya Mill.2,900000 kwa kikosi cha timu ya Jeshi la Zima moto Mkoani Iringa
Akimkabidhi Mratibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Iringa, kwa niaba ya Hans Popo,Siza Hans alisema kuwa ameamua kuisaidia timu hiyo vifaa vya michezo ili iweze  kucheza kwa bidii na hatimae timu iweze kusonga mbele.
“Sote tunatambua  umuhumu wa michezo katika jamii,hivyo tumeona tutoe msaada huu ili uisaidia timu ya zimamoto kujiweka fiti katika suala zima la afya, kiakili. Tunajua ugumu na shida ambazo zinakaibili timu nyingi za soka na michezo mingine mbalimbali hapa Nchini ninawaomba na wadau wengine waendelee kujitolea ili kutatua changamoto hizo’’’’’’’alisema Sinza
Aidha aliitaka Serikali kurudisha michezo  katika Shule za Msingi na Sekondari ili  wananfunzi mara wamalizapo  waweze kuendelea kuipenda michezo na hatimae kuwa wachezaji wazuri hapo baadae.
  
‘’’Kitendo cha serikali kuondoa michezo katika shule za msingi
 na sekondari  Nchini ndiyo chanzo kikubwa cha kuyumba kwa michezo mbalimbali nchini Tanzania. Endapo Serikali itarejesha michezo shuleni ,kutakuwa na Mwamko  mkubwa wa michezo na hatimae vipaji vingi vitaibuka.’’’’’alisema
Aliongeza  kuwa wakati michezo ilipokuwa ikifundishwa katika shule za msingi na sekondari mwamko  wa kuipenda michezo ulikuwa mkubwa kwa kila mwananchi  na kiwango
cha michezo kilionekana tofauti na hivi sasa .
Kwa upande wake Mratibu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Iringa,kamanda KennedyKomba, akimshukuru Zakaria Hans Popokwa msaada wa seti nne za jezi na soksi nakusema kuwa msaada huo,alisema kuwa vifaa hivyo vimekuja kwa wakati muafaka kutokana na  kikosi hicho kuwa
 katika mazoezi makali  ya kujiandaa na mashindano yanayotarajia yatakayfanyika Mkoani hapa hivi karibuni.
 Komba alisema hapo awali timu hiyo ilikuwa inakabiliwa na uhaba wa vifaa vya Michezo,hivyo  msaada huo umewapa
moyo na  nguvu na kuwafanya  waone kuwa  jamii inakitambua kikosi cha zimamoto katika suala la kukuza michezo kwa kikosihicho. 
Hilaly Kobelo ni Mkaguzi Msaidizi wa Zimamoto mkoa wa Iringa,ambae pia ni nahodhawa wa kikosi  cha Timu hiyo alisema kuwa, kikosi hicho kilikuwa kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wavifaa vya michezo hivyo msaada huo utawasaidia katika kujiandaa na michezombalimbali.
Kobelo alisema  mikakati ya kuanza kuipandisha daraja timu hiyo hadi kufikiangazi ya ligi kuu imeanza, na hii itawasaidia hata kupata wadhamini endapo timu hiyo itafanya vizuri katika mashindano yajayo watakayoshiriki
MWISHO














0 maoni:

Chapisha Maoni