Jumamosi, 29 Oktoba 2016

Naibu Waziri wa Afya Dk.Kigwangalla: Serikali itaendelea kupambana na Saratani ya Matiti nchini


Posted by Esta Malibicheon News
Naibu waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla amebainisha kuwa  Serikali itaendelea kupambana kwa hali na mali kuhakikisha wanapambana na tatizo la ugonjwa wa Saratani ya Matiti hapa nchini ikiwemo kutoa elimu na tiba kwa Wananchi wake.
Hayo ameyasema mapema leo Oktoba 29.2016 Jijini Dar es Salaam wakati wa matembezi ya hisani ya kuhamasisha uchunguzi wa saratani ya matiti yaliyoandaliwa na Taasisi ya Saratani ya Hospitali ya Ocean Road jijini Dar es Salaam ambapo huu ni mwaka wa nne tokea yameanzishwa.
Ambapo akihutubia wananchi mbalimbali pamoja na vikundi vya wataalamu na wadau wa masuala ya mapambano ya Saratani hapa nchini, Dk.Kigwangalla amesema kuwa jitihada mbalimbali zinafanywa na Serikali kwa kushirikiana na wadau wengine ili kutokomeza kabisa ugonjwa huo.
 “Kwa hapa kwetu Tanzania wagonjwa wa Saratani ya Shingo ya kizazi ni wengi zaidi kuliko wagonjwa wa saratani ya matiti. Kila mwaka  takribani ya watu 44,000 wanapata saratani lakini hawafiki Hospitali kwa sababu mbalimbali na ni asilimia 10 tu ya wagonjwa ndio wanaofika Hospitali kwa uchunguzi na matibabu” alieleza Dk.Kigwangalla wakati wa kusoma hotuba yake hiyo.
Hata hivyo amewaondoa hofu wananchi juu ya dhana kuwa mtu haponi ugonjwa huo  jambo ambalo si kweli  zadi ni ni elimu inahitajika zaidi pamoja na tiba.
“Tuwe na taratibu za kufanya uchunguzi wa mara kwa mara. Tuachane na dhana potofu kama sratani haitibiki, Jitokeze kucheki tatizo na wataalam watakupa huduma kukabiliana na ugonjwa huo. Kama tulivyoshuhudia baadhi ya waliotoa shuhuda leo hapa” alimalizia Dk.Kigwangalla.
Awali katika tukio hilo, Dk.Kigwangalla na wageni wengine mbalimbali waliweza kufanya matembezi ya hisani ya zaidi ya KM 4. Yaliyoanzia katika viunga hivyo vya Hospitali ya Ocean Road kasha kuzunguka katikati ya Jiji la Dar es Salaam.
Fedha mbalimbali zilichangishwa katika tukio hilo.

0 maoni:

Chapisha Maoni