Jumamosi, 29 Oktoba 2016

MUSWADA WA SHERIA YA HUDUMA ZA HABARI UNALENGA KULETA HESHIMA KWA WATANZANIA.

Posted by Esta Malibiche on Oct 29.2016 in NEWS

b1 b2
Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii wakiendelea na kazi ya kuchambua maoni yaliyotumwa na wadau wa habari ili kuboresha Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari leo mjini Dodoma.
(Picha na MELEZO)
Na Eleuteri Mangi-MAELEZO, Dodoma
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii inaendelea na kazi yao ya kutunga Sheria ya Huduma za Habari kwa kutumia maoni yaliyowasilishwa na wadau mbalimbali na kuwasilisha Serikalini kabla ya kupelekwa Bungeni ili  muswada ukajadiliwe na Wabunge na hatimaye kupatikana Sheria ya Habari ambayo inalenga kuleta heshima kwa Watanzania.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Peter Serukamba amebainisha hayo leo mjini Dodoma alipokuwa akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kabla ya Kamati hiyo kuendelea na kazi yake ya kuchambua maoni yaliyotumwa na wadau wa habari ili kuboresha Muswada huo kabla ya kuwasilishwa Bungeni kusomwa kwa mara ya pili.
Serikali imekuwa ikiwasikiliza wadau wa habari kwa muda mrefu licha ya kuwa na tabia ya kutokuwasilisha maoni yao kila mara wanapoomba kupewa muda wa kutoa maoni yao juu ya kuboresha Muswada wa Sheria ya Huduma za Habari nchini.
 “Ni vizuri ifahamike, huu ndio umekuwa mchezo wa Muswada huu tangu mwaka 1993, kila mara Muswada ulipokuja Bungeni, wadau walisema hawapo tayari wanasema utoke” alisema Mhe. Serukamba.
Aidha, Mhe. Serukamba amesisitiza kuwa huo umekuwa ni mtindo wa wadau hao kwa miaka zaidi ya 22 sasa ambapo Serikali imekuwa imekuwa ikiwasililiza kila waliposema hawapo tayari, muswada huo ulitolewa Bungeni.
Kufuatia tabia ya wadau kutokuwasilisha maoni yao kwa kisingizio cha kutopewa muda Mhe. Serukamba amesisitiza kuwa kamati itaendelea kujadilia maoni yaliyowasilishwa kwako na kuahidi kutunga Sheria itayozingatia na kujali maslahi ya wadau wote wa habari ili kuufanya Muswada huo kuwa wenye tija kwa wananchi na taifa kwa kuleta  mabadiliko katika tasnia ya habari nchini.
Ili kusimamia nia na maslahi ya wadau na taifa, Serikali imeuleta tena Muswada huo Bungeni ambapo Kamati ya Huduma za jamii inaendelea kuujadili na kuchambua maoni yaliyowasilishwa na wananchi pamoja na wadau wa habari kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa maandishi kupitia barua pepe ya Bunge cna@bunge.go.tz
Mwenyekiti wa Kamati hiyo amewataja wadau waliothibitisha kupokea barua ya mwaliko wa kuleta maoni yao kwa Kamatikuwa ni pamoja na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), MCT, LHRC, UTPC pamoja na Pili Mtambalike.

0 maoni:

Chapisha Maoni